• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Historia

Historia ya Mkoa wa Geita

Mkoa wa Geita ulianzishwa rasmi kwa Tangazo la Serikali namba 72 la tarehe 02 Machi, 2012, na kuzinduliwa tarehe 08, Novemba, 2013 na Mheshimiwa DKT Jakaya Mrisho Kikwete Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mkoa huu ulitokana na sehemu ya Mikoa ya Mwanza, Kagera na Shinyanga ambapo upande wa Magharibi na Kusini unapakana na Mkoa wa Kagera, upande wa Kusini na Kusini Mashariki unapakana na Mkoa wa Shinyanga na Mwanza kwa upande wa Kaskazini unapakana na Ziwa Victoria.

Umbile la Mkoa na Maeneo ya Utawala

Mkoa huu una eneo au ukubwa wa kilometa za mraba 21,879 (Geita 6,375 km2, Bukombe 6,798 km2, Chato 3,572 km2, Mbogwe 3,684 km2, na Nyang`hwale 1,450 km2), kati ya hizo kilomita za mraba 19,933 niza nchi kavu na kilomita za mraba1,946 ni za maji.

Mkoa una Wilaya tano (5), Majimbo saba (7) ya Uchaguzi, Halmashauri sita (6), Mji mdogo 1, Tarafa23, Kata 122, Vijiji 474, Vitongoji 2,219 na Mitaa 65. Wilaya hizo ni Geita, Nyang‟hwale,Chato, Bukombe na Mbogwe.

Mkoa unajumuisha  Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Halmashauri za Wilaya za Geita, Nyang’hwale, Chato, Bukombe na Mbogwe. Kuanzishwa kwa Mkoa huu kumesaidia kuharakisha upelekaji wa huduma za kijamii, kiuchumi na maendeleo kwa wananchi.

Idadi ya Watu

Kwa mujibu wa sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2022, Mkoa una wakazi wapatao 2,977,608 ambapo wanaume ni 1,463,764 na wanawake ni 1,513,844

.

Idadi ya Watu Katika Halmashauri zote  kwa Mwaka 2022








JINA LA HALMASHAURI
IDADI YA WATU
IDADI YA WANAUME
IDADI YA WANAWAKE
IDADI YA KAYA
UWIANO WA JINSIA

Wilaya ya Geita
1,035,214
507,788
527,426
198,797
97

Manispaa ya Geita
361,671
177,271
184,400
78,537
96

Nyang'hwale
225,803
113,495
112,308
36,159
101

Mbogwe
362,855
179,157
183,698
63,635
98

Bukombe
407,102
199,915
207,187
74,664
96

Chato
584,963
286,138
298,825
110,156
96









Chanzo: NBS, 2022

Hali ya Hewa

Mkoa unapata mvua za kutosha kuanzia milimita 900 hadi 1200 na joto la wastani la nyuzi 22 hadi 30 kwa mwaka. Aidha, Mkoa umekuwa ukipata mvua za vuli katika kipindi cha kuanzia Septemba hadi Desemba na mvua za masika kuanzia mwishoni mwa mwezi Februari hadi Mei. Pia, kipindi cha kiangazi huanza mwanzoni mwa mwezi Juni hadi Septemba kila mwaka na unyevu wa kati ya asilimia 35 na 60.

Shughuli Za Kiuchumi na Pato la Mkoa

Wakazi wa Mkoa wa Geita wanajishughulisha na shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ikiwa ni pamoja na kilimo, ufugaji wa mifugo mbalimbali na nyuki, uvuvi, uchimbaji madini pamoja na biashara ndogo ndogo. Aidha, Sekta ya kilimo ina changia takribani asilimia 70 ya pato la Mkoa wa kati shughuli nyingine za kiuchumi zinachangia asilimia 30. Kwa mujibu wa takwimu kutoka NBS mwaka 2013 zinaonesha kuwa mchango wa Mkoa wa Geita katika pato la taifa umefikia shilingi bilioni 1,584 wakati Pato la mwananchi ni Shilingi 910,824.

Fursa za Uwekezaji zilizopo Mkoani Geita

Mkoa unafanya vizuri katika Uwekezaji na una zitangaza fursa mbali mbali zilizopo. Fursaza Uwekezaji katika Mkoa zipo katika Sekta za:- Kilimo, mifugo, madini, uvuvi, ujenzi, misitu na utalii. Pia hupatikana katika Sekta za Usafirishaji na Nishati. Mkoa unafanya jitihada mbalimbali za kuvutia wawekezaji na kuzinadi fursa za uwekezaji zilizopo ili wawekezaji waje kuwekeza na hatimaye kuongeza kasi ya maendeleo ya Mkoa. Baadhi ya wawekezaji ni Ukurwa Investments, Lake Gas, Lenny Hotel Limited, Waja Schools & Hospital, Makoye Hospital, Chobo Investiment, National Housing Cooperation, GGM na VETA.

Orodha ya Viongozi wa Mkoa wa Geita toka Kuanzishwa Kwake Mwaka 2012

1. Wakuu Wa Mikoa

NA.
JINA
CHEO
MWAKA
1.
Mhe. Magalula Said Magalula
Mkuu wa Mkoa
2012-2014
2.
Mhe. Fatma A. Mwassa
Mkuu wa Mkoa
2014-2016
3.
Mhe. Meja Jenerali (Mst) Ezekiel E. Kyunga
Mkuu wa Mkoa
2016-2017
4.
Mhe. Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi
Mkuu wa Mkoa
2017-2020
5.
Mhe. Rosemary Staki Senyamule
Mkuu wa Mkoa
2020-2022
6
Mhe. Martine Shigela
Mkuu wa Mkoa
2022


2.Makatibu Tawala wa Mkoa

NA JINA CHEO MWAKA
1 Ndugu. Severine Kahitwa Katibu Tawala Mkoa 2012 - 2014
2 Ndugu. Charles A. Pallangyo Katibu Tawala Mkoa 2014 -2016
3 Ndugu. Selestine M.Gesimba Katibu Tawala Mkoa 2016 -2018
4 Ndugu. Denis I. Bandisa Katibu Tawala Mkoa 2018 - 2020
5 Ndugu. Mussa Chogero Katibu Tawala Mkoa 2020 - 2022
6 Prof. Godius W. Kahyarara Katibu Tawala Mkoa 2022 - 2023
7 Ndugu. Mohamed  J. Gombati Katibu Tawala Mkoa 2023 -

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Wafanyabiashara Wadogo Wahamasishwa Kujisajili

    May 15, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa