• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ahsante Serikali ya Awamu ya Sita- RC Shigela

Posted on: September 11th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoanzishwa na Rais wa awamu ya tano Hayati John Pombe Magufuli katika Mkoa wa Geita.

Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo hivi karibuni alipokuwa akitembelea na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbli inayoendelea katika Wilaya ya Chato mkoani Geita pamoja na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara kwa lengo la kusikiliza kero zinazowasumbua na kutafuta namna ya kuzitatua.


Akitembelea majengo ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha Kampasi ya Geita ,Mkuu wa Mkoa wa Geita ametoa wito kwa wanafunzi wenye sifa walioko Geita na mikoa ya jirani kutohangaika kusafiri kufuata elimu mbali bali wajiunge na Chuo cha IFM tawi la Geita ambapo udahili wa  wanafunzi kuanzia mwaka huu wa masomo 2024/2025 umeanza. Pia amewakumbusha wananchi kuchangamkia fursa mbalimbali za kibiashara kama maduka, hoteli, migahawa, stationary nk zitakazopatikana chuoni hapo baada ya kufunguliwa.

Akikagua ujenzi wa Hoteli ya nyota tatu Burigi-Chato, Mhe. Shigela ametoa pongezi kwa Hifadhi za Taifa Tanzania kwa kufikisha asilimia 70% ya ujenzi na kutoa ombi kwa TANAPA kutoa fedha kwa wakati ili ujenzi wa hoteli hiyo uweze kukamilika na kuanza kutoa huduma zitakazowezesha kukuza utalii na kuongeza pato la Taifa, kuondoa changamoto ya malezi kwa wageni, kutoa fursa ya ajira kwa wananchi na kukuza uchumi wa Wilaya ya Chato na Mkoa wa Geita kwa ujumla kupitia sekta ya utalii.

Mbunge wa jimbo la Chato Mhe. Medard Kalemani ametoa ombi kwa uongozi wa TANAPA kuwapatia kipaumbele cha ajira za kudumu wakazi wa wilaya ya Chato mradi huo utakapoanza kazi ili mwananchi mmoja mmoja aweze kujipatia maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amemshuru pia Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuanzisha ujenzi wa Mataba ya kisasa  ambayo ni ya kwanza kwa ukubwa katika kanda ya ziwa na kutoa agizo kuwa Maktaba hiyo itakapokamilika itumiwe na watu wa rika zote.


Mhe. Shigela ameeleza wananchi kuwa changamoto ya uhaba wa maji itafika mwisho baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji katika kata ya Bukome wilayani Chato ikiwa ni sehemu ya mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa katika miji 28 Tanzania kwa shilingi Bilioni 38.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa