• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Binti Shanti Mahudi Aiongoza Menejimenti ya Mkoa kwa Saa 1, Atoa Rai kwa Watendaji

Posted on: October 19th, 2023

Na Boazi Mazigo – Geita RS

Ikiwa ni mwezi ambao ndani yake ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike duniani, mwanafunzi  wa kidato cha tatu kutoka shule ya Sekondari Nyanza iliyopo halmashauri ya mji Geita, Bi.Shanti Mahudi (16) ameongoza kikao cha menejimenti ya ofisi ya mkuu wa mkoa Geita ikiwa ni utekelezaji wa programu maalumu inayoratibitibiwa na shirika lisilo la kiserikali la Plan International Tanzania ijulukanayo kama Girls Takeover, programu ambayo hufanyika kwa kumwezesha msichana kuwa kiongozi ndani ya muda mchache akiigiza kutekeleza majukumu ya kiongozi husika kwa lengo la kumjengea uwezo na ujasiri.

Bi.Shanti ameongoza kikao hicho Oktoba 19, 2023 katika ofisi ya Katibu Tawala Mkoa ambapo ameketi na wakuu wa idara na vitengo mbalimbali akizungumza nao akisisitiza juu ya uzingatiaji mahitaji maalumu ya mtoto wa kike kwenye shule zote ikiwemo maji safi na salama, taulo za kike (Sodo) pamoja na chumba maalum cha kujihifadhi mabinti wanapokuwa kwenye siku zao za hedhi n.k.

“niwashukuru kwa mwitikio wenu na niombe muwasaidie wasichana kupata maji safi na salama, ulinzi, taulo za kike (sodo). Mtambue yakuwa, watoto wa kike wanapotoka nyumbani kuelekea shule, hukutana na vishawishi vingi njiani, hivyo ni muhimu kuwaongezea ulinzi kwa kujenga mabweni kwenye shule”, alisema Bi.Shanti.

Bi.Shanti alihitimisha kwa kusisitiza juu ya uendelezwaji vipaji kwa watoto wa kike ikiwemo kuwajengea vyumba maalum bila kusahau waalimu wenye vipaji na upatikanaji wa vifaa vya michezo. Aidha, aliomba viongozi kusaidia kuondoa mtazamo hasi unaomtafsiri mtoto wa kike kama hastaili kupewa elimu bali wasaidiwe kupata elimu kwakuwa nao wana mchango mkubwa ikiwemo kuwa viongozi wakubwa nchini.

Kwaniaba ya menejimenti ya ofisi ya mkuu wa mkoa Dkt.Omary Sukari ambaye ni kaimu katibu tawala mkoa alisema, yote yaliyosemwa na Bi.Mahundi yatashughulikiwa na yamekuwa yakipewa msukumo kuanzia ngazi ya mkoa hadi halmashauri huku akisema, “nikushukuru kwa ziara yako, na nikuhakikishie yote uliyotueleza kila mmoja kwenye nafasi yake ataenda kuyatekeleza; na nichukue fursa hii kumpongeza mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwarejesha watoto wa kike waliopata ujauzito wakiwa masomoni na kama mkoa tutaendelea kumhakikishia mtoto wa kike ulinzi ili aweze kusoma na kufikia malengo yake”.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa