• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Dkt.Biteko Akemea Utoroshaji wa Madini Nchini

Posted on: May 29th, 2022

Waziri wa Madini Mhe.Dkt.Doto Biteko amekemea utoroshwaji wa madini unaofanywa na baadhi ya wafanya biashara wasio waaminifu ambao bado hutorosha madini hayo.

Mhe. Biteko ameyasema hayo leo kwenye ziara ya kikazi Mkoani Geita katika eneo la Lwamgasa, Halmashauri ya Willaya ya Geita baada ya kutembelea Mgodi mdogo wa Nassoro Juma wa mwananchi, mialo miwili pamoja na mgodi wa mfano wa Lwamgasa wa serikali chini ya STAMICO

"serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassan imepunguza tozo mbalimbali kwa lengo la kuweka mazingira bora kwenye sekta ya madini"amesema Dkt. Biteko

Pia akatumia nafasi hiyo kutoa maelekezo mengine kwenye sekta anayoisimamia akisema.

“tayari tumewakamata watu 8 kwa tuhuma za utoroshaji madini, na nitoe onyo kwa mnaoendelea kwani mnatorosha madini kwa ajili ya nini wakati tayari serikali inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassani ilikwisha kutengeneza mazingira mazuri kwa kupunguza tozo mbalimbali?” alisema Waziri Biteko

Pia amempongeza mchimbaji mdogo Nassoro Juma ambaye amekuwa akifanya kazi vizuri huku akiwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi pamoja na jamii na ndiyo maana anachangia CSR,


Waziri Biteko alitoa agizo kwa maafisa madini wote nchini kuhakikisha wananchi kuacha kuweka mialo kwenye mnyumba zao na kuelekeza suala hilo lisimamiwe na serikali ya wilaya chini ya mkoa na kwamba kuanzia sasa yatengwe maeneo ambapo mialo yote itakaa hapo, itasajiliwa na wenye mialo nao wahakikishe wanaweka rekodi za dhahabu wanayoipata kwani imeonekana kwa kiasi kikubwa mapato yatokanayo na dhahabu inayotokana na Zebaki yameshuka kwa kiasi kikubwa kutokana na utoroshwaji wake. Vilevile aliiagiza STAMICO kuongeza ukubwa wa huduma baada ya mwitikio wa wateja kwani awali mgodi wa Lwamgasa uliwekwa kwa majaribio hivyo unazidiwa kwa sasa.


Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa geita Mhe.Rosemary Senyamule alisema anaipongeza Wizara ya Madini kwa kuutambua mkoa wa geita kuwa ni mkoa unaoongoza kwa uzalishaji wa madini ya dhahabu na kwamba dhamira iliyopo ni kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha Madini ya Dhahabu na ndiyo maana kwa kuanzia mkoa umejenga soko kubwa la Madini na unaendelea na jitizada kwa kushirikiana na wizara ili kuwasaidia wachimbaji wadogo ili waboreshe teknolojia ya uchimbaji.


Awali, Waziri Biteko alipata wasaa wa kusikiliza kero, maoni na pongezi kutoka kwa wananchi na wachimbaji wa Lwamgasa na kisha kuahidi kuchukua hatua mbalimbali katika utatuzi ya yale yaliyoonekana kuwa mahitaji ya wananchi hao ikiwamo kuomba kuruhusiwa kuchimba kwenye maeneo yaliyotolewa kwa vikundi na kushindwa kuyaendeleza.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa