• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Epukeni Tabia ya Utoroshaji Mapato- RAS Geita

Posted on: July 1st, 2025



Katibu Tawala Mkoa wa Geita Ndugu Mohamed Gombati amewataka watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita kudhibiti mianya ya udokozi na utoroshaji wa mapato ya Serikali na kuepuka kuhujumu jitihada za makusanyo ya mapato ya Halmashauri.


Ndg. Gombati ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na watumishi wa Manispaa ya Geita katika kikao kazi kilichofanyika tarehe 30 Juni 2025 kwenye ukumbi wa mikutano katika Viwanja vya Maonesho vya Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Bombambili, Geita mjini.


Katibu Tawala Mkoa wa Geita ameeleza kuwa watumishi wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu ambao wanahusika na ukusanyaji mapato waepukane na tabia ya kutoa siri ya mikakati ya ukusanyaji mapato iliyowekwa na Serikali Pamoja na kuachana na desturi ya kuomba rushwa kwa wananchi wakati wa utoaji huduma.


Sambamba na hilo Ndg. Mohamed Gombati amewakumbusha watumishi hao kufanya kazi kwa upendo, umoja na ushirikiano pasipo kusahau kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za utumishi wa Umma Pamoja na kusimamia misingi ya utawala bora na maadili ya Utumishi wa Umma.


“Watumishi wenzangu mnatakiwa kutambua kuwa kila mmoja wenu kulingana na kada yake ni mtu muhimu katika kuhakikisha shughuli za Serikali zinafanywa kikamilifu na kwa kuheshimiana pasipo kusahahu viapo vya kazi na utunzaji wa siri za ofisi kwa lengo la kuongeza umakini wa kazi Pamoja na kuiwezesha Halmashauri kutimiza vyema majukumu yao”. Aliongeza Katibu Tawala Mkoa wa Geita.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita Ndg. Yefred Myenzi ametoa shukrani za dhati kwa Katibu Tawala Mkoa kwa kuketi Pamoja na watumishi wake katika kikao ambacho kimetoa fursa kwa watumishi wote kutoa changamoto na ushauri unaolenga kuboresha utendaji kazi na kusaidia kuchochea maendeleo ya Manispaa ya Geita na Mkoa wote kwa ujumla.





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Epukeni Tabia ya Utoroshaji Mapato- RAS Geita

    July 01, 2025
  • Bukombe na Mbogwe Zapongezwa Kwa Kupata Hati Safi

    June 23, 2025
  • Jamii Yatakiwa Kulinda Haki za Watoto

    June 20, 2025
  • Jamii Yatakiwa Kulinda Haki za Watoto

    June 20, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa