• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

GEITA KUTUMIA KANUNI MPYA ZA CSR ZA MWAKA 2023

Posted on: August 11th, 2023

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan imeendelea kutoa suluhu ya mambo mbalimbali ili kuongeza ufanisi wa shughuli ikiwemo upande wa sekta ya madini.

Hayo yalibainika Agosti 10, 2023  wakati mkuu wa mkoa Geita mhe.Martine Shigela akifungua kikao maalum kwa ajili ya kuelimishana juu ya Kanuni za wajibu wa wamiliki wa leseni za madini kwa jamii CSR za mwaka 2023 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa Geita.

Akizungumza kabla ya ufunguzi wa kikao na baada ya majadiliano, RC Shigela alisema, “tunaipongeza serikali chini ya Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha upatikanaji wa kanuni hizi, lakini pongezi nyingine zimfikie waziri wa madini Mhe.Dkt.Doto Biteko pamoja na wizara kwa jitihada hadi leo ili kutatua changamoto za upatikanaji wa kanuni za CSR. Ni matarajio yangu kuwa mpango wa CSR mwaka 2024 utazingatia kanuni hizi”.

RC Shigela aliongeza kwa kumpongeza katibu tawala mkoa Prof.Godius Kahyarara pamoja na mgodi wa GGML kwa kushirikiana kuandaa kikao hicho, kisha kuwasihi washiriki wa kikao hicho kuanza mara moja matumizi ya kanuni hizo na kwamba endapo changamoto zitajitokeza, kanuni hizo zitaboreshwa zaidi.

Naye mwenyekiti wa CCM mkoa Geita Nicholaus Kasendamila alisema,”ninawashukuru wote wenye uchungu na Geita yetu. Kanuni hizi zikatusaidie kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zatukabili”.

Akiwasilisha kanuni hizo, afisa biashara madini mwandamizi idara ya ukaguzi, biashara ya madini, ushirikishwaji wa Watanzania na CSR bw.Issa Lunda alisema, miongoni mwa kanuni hizo ni ile ambayo 40% itatengwa kwa ajili ya miradi ya kijiji au mtaa ambapo shughuli za madini zinafanyika na 60% itatengwa kwa ajili ya miradi ya halmashauri ya wilaya, mjin manispaa au jiji husika ambako shughuli za madini zinafanyika.

Bw.Lunda aliongeza kuwa ni muhimu CSR kuzingatia kubadilisha maisha ya wananchi walio maeneo yaliyo na uchimbaji akitolea mfano wa kuhama kwenye kilimo cha umwagiliaji kuliko kutegemea mvua. Alihimiza uaminifu na uadilifu kwa maofisa wanaosimamia CSR ili kuleta tija kwa wananchi huku akiainisha changamoto ambazo zilikuwa zinatokana na kutokuwa na kanuni kama miradi kutotekelezwa kwa wakati, kupishana kwa mtazamo kati ya halmashauri na migodi pamoja na uelewa mdogo wa masuala ya CSR.

Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe wakiwemo wajumbe wa kamati ya usalama mkoa, sekretarieti ya mkoa, wabunge, kamati ya usalama wilaya, madiwani, watendaji kata pamoja na wakuu wa idara halmashauri ya wilaya ambapo Agosti 11, 2023 ni zamu ya halmashauri ya mji Geita zote zikiwa wilaya ya Geita.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa