• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Geita yaadhimisha Miaka 60 ya Uhuru na 59 ya Jamhuri

Posted on: December 8th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Geita, Mhe. Rosemary Senyamule amewataka viongozi wa dini pamoja na viongozi wa siasa  kushirikiana kwa pamoja kuwaunganisha watanzania kwa lengo la kudumisha  amani na mshikamano uliopo nchini kama tunu ya taifa.

Amesema hayo Leo tarehe 08.desemba 2021 wakati akiwaongoza wananchi wa mkoa wa Geita kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru na 59 ya Jamhuri hafra hiyo imefanyika katika ukumbi wa GEDECO mjini Geita amewataka viongozi kuwaunganisha watanzania ili kulinda umoja na mshikamano uliopo nchini kama tunu ya taifa ili kuenzi amani na mshikamano uliopo nchini.

Aidha, Mhe. Mkuu ametoa wito kwa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kwalengo la kujiletea maendeleo.

 "Nitoe wito kwenu kila mmoja afanye kazi kama vile atakufa leo, ili uhuru huu uendelee kuleta maana na kuonesha thamani ni maendeleo hivyo kila mtu afanye kazi kwa kujituma kwa bidii kwani uchumi haukuwi kwa kulala usingizi",amesema.

Vilevile, Mhe. Senyamule amesema baada ya baba wa Taifa viongozi waliofuata waliendelea kuboresha Miundombinu ya barabara na huduma zingine za kutolea huduma za afya kwa wananchi kwa lengo la kukuza uchumi wa taifa.

Hata hivyo mkuu wa mkoa amewapongeza wananchi wa Geita kwa kuishi kwa kudumisha amani. "Historia inaonesha miaka michache iliyopita Geita haikua salama kutokana na matukio ya mauaji ya vikongwe na albino lakini sasa mkoa upo salama hivyo tuendelee kuienzi amani na tukatae kujiingiza kwenye matendo yote yanayohatarisha amani ya nchi." Amesema.

Vile vile Mhe Mkuu wa Mkoa wa Geita amewataka  wananchi wa mkoa huo kusimamia na kuelimisha wananchi kwa lengo la kuchukua tahadhari kwa kutunza mazingira pamoja na kuhifadhi vyanzo vya maji ili kuondokana na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi.

Hata hivyo chanjo ya hiyari ya Ugonjwa wa Uviko 19 ameigusia na ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa ya kuchanja kwa hiyari ili kujikinga na maradhi hayo ambayo hivi sasa tupo kwenye wimbi la nne la ugonjwa huo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe, Wilson Shimo ametumia nafasi hiyo  kwakuwataka wananchi kudumisha umoja pamoja na kufanya kazi kwa bidii kama ngao ya kujitegemea kwenye wakati huu ambapo Taifa limefikisha miaka 60 ya Uhuru.

 "Akina mama wanakopesheka maana wanaongoza kwa urejeshaji wa mikopo kwenye Halmashauri haya ni matunda ya Uhuru wa Tanzania." Mhe. Martha Mkupasi Mkuu wa Wilaya ya Chato.

Aidha, Mhe. Mkupasi amesema kuwa kuelekea Miaka 60 ya Uhuru nchini, kumekua na ongezeko la viongozi wanawake na akabainisha kuwa akinamama ni nguzo imara na ndio viongozi kwenye ngazi za familia.

Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe, Mhe. Mhandisi Charles Kabeho amesema hali ya usafiri  zamani ilikua ya shida lakini kwa sasa watu wanasafiri kwa urahisi kutokana na kuimarishwa kwa Miundombinu hapa nchini.

 "Kila mtanzania ana wajibu wa kufikiri ana wajibu gani wa kulitumikia Taifa lake la Tanzania ili kupata mafanikio. " Eng. Kabeho.

Kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Katibu Tawala wa Wilaya, Ndugu Fabiani Yinza amewapongeza viongozi wa awamu zote za Uongozi hapa nchini  kwa kuliletea taifa  maendeleo.

"Bidhaa zetu zitashuka bei sana kutokana na uwepo wa reli ya kati na vijana wengi watapata ajira kupitia uwepo wa reli hii ya kati." Amesema.

Bi. Rhoda Simon, Mwalimu mstaafu aliyezaliwa tarehe 09 Desemba 1961 amemshukuru Mungu kwa uhai hadi anashuhudia nchi ikiadhimisha miaka 60 ya Uhuru na amesema  miaka ya nyuma Geita mjini palikua na shule moja tu ya Sekondari ya wasichana lakini sasa shule za Sekondari ni nyingi jambo linalopelekea wanafunzi kutembea muda mfupi kufika shuleni.

Maadhimisho haya yameenda sambamba na Dua na Sala Maalum ya kuwaombea Viongozi na Taifa kuendelea kuwa na amani na kuwa Nchi yenye mafanikio na hatimaye liweze kukua kiuchumi siku hadi siku.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa