• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Jamii Yatakiwa Kulinda Haki za Watoto

Posted on: June 20th, 2025


Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Mheshimiwa Grace Kingalame ametoa rai kwa jamii kuhakikisha wanalinda haki za watoto na kutimiza wajibu wao katika kujenga maisha ya watoto yanayoendana na mila na desturi za kiafrika.

Mhe. Kingalame ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela wakati wa maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika kimkoa hivi karibuni katika viwanja vya Sabasaba Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale.

Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale amewakumbusha wazazi, walezi na Taasisi zisizo za Kiserikali zinazoshughulika na masuala ya haki za watoto kuwajibika kutekeleza haki tano za msingi za mtoto ambazo ni Haki ya kuishi, kuendelezwa, kulindwa, kushirikishwa na kutobaguliwa.

“Kila mwanajamii ana jukumu la kuzuia ukiukwaji wa maadili na kuwafundisha watoto kuishi katika misingi na tamaduni za kitanzania kwa lengo la kupata kizazi endelevu kitakachoepukana na mmomonyoko wa maadili katika jamii. Mila na desturi za kitanzania zinapaswa kutambuliwa na kuendelezwa kwa kuwa zina manufaa katika kulinda na kuendeleza maadili mema ya Taifa letu”. Aliongeza Mhe. Kingalame.

Mhe. Kingalame alitumia fursa hiyo pia kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ifikapo mwezi Oktoba 2025.

Katika risala iliyosomwa na watoto wameomba Serikali na jamii kwa ujumla kuendelea kutokomeza changamoto ambazo zinawakabili watoto ikiwa ni pamoja na ongezeko la watoto wanaoishi mitaani, watoto kukosa maadili na malezi bora kutoka kwa wazazi/walezi wao, utoro mashuleni unaosababishwa na ukosefu wa mahitaji ya msingi kwa watoto, vitendo vya ubakaji na ulawiti vinavyofanywa kwa watoto, mimba katika umri mdogo, baadhi ya wazazi kuozesha mabinti wenye umri mdogo na wazazi/ walezi kutotimiza mahitaji ya msingi ya watoto katika familia zao.

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka 2025 yameongozwa na Kauli mbiu isemayo “ Haki za Mtoto: Tulipotoka, Tulipo na Tuendako.”



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Bukombe na Mbogwe Zapongezwa Kwa Kupata Hati Safi

    June 23, 2025
  • Jamii Yatakiwa Kulinda Haki za Watoto

    June 20, 2025
  • Jamii Yatakiwa Kulinda Haki za Watoto

    June 20, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa