• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Siasa ya CCM Yawapa Joto la Elimu Kidato cha 5 Mbogwe

Posted on: August 23rd, 2023

Na Boazi Mazigo- Geita RS

Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Geita kimeendelea kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi kwa vitendo kwa kupita kukagua na kufuatilia utekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo kikihimiza ubora na thamani ya miradi. 

Hayo yamedhihirika Agosti 23, 2023 wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa Geita walipotembelea na kuwatia joto la mafanikio wanafunzi wapya wa kidato cha tano wa shule ya sekondari Mbogwe ambapo wajumbe hao walitumia nafasi hiyo kuwaasa wanafunzi hao kutumia nafasi walioipata ili kuzifikia ndoto zao.

Akiongea na wanafunzi hao, mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Mkoa Geita Nicholaus Kasendamila alisema "unayesoma ni wewe, shughulika na masomo na yale mapungufu unayoyaona waachie viongozi wayashughulikie. Kwa kuwa mmepata bahati ya kupata Miundombinu mizuri, someni na tutapenda kuna wote mnafauru"

Vilevile Mwenyekiti Kasendamila alisisitiza juu ya wahandisi kuendelea kusimamia kwa ukaribu ujenzi wa miradi ili kudumisha ubora na tija kwa ustawi wa nchi hii ikiwa pia ni kumuunga mkono kwa vitendo Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia usimamizi ulio mzuri wa miradi

Nao wajumbe wengine kwa wakati tofauti, waliwapongeza wanafunzi hao kwa kufaulu na kuchaguliwa kujiunga na shule hiyo, wakiwataka kuongeza juhudi na kutilia mkazo suala la elimu ili wawe viongozi wa taifa hapo baadaye.

Kwa upande wake Mhe.Cornel Magembe ambaye ni mkuu wa wilaya Geita kwaniaba ya Mkuu wa mkoa geita alisema, "kwaniaba ya serikali mkoani hapa, nawakaribisha sana, na serikali inaendelea kuboresha Miundombinu mbalimbali kupitia fedha zinazoendelea kuletwa na Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Nao bw.Seth Bwire na bi.Felister Vicent ambao ni wanafunzi wa kidato cha tano walitumia fursa hiyo kukishukuru Chama Cha Mapinduzi CCM pamoja na viongozi wa serikali walioambatana nao na kuwaahidi kusoma kwa bidii na kwamba watakapomaliza elimu yao wanaamini watafaulu kwa kishindo.

Kamati hiyo imetembelea na kukagua miradi ya Shs.1,690,657,756.06 ya sekta ya elimu na afya na kuhimiza wahandisi kusimamia miradi kwa ukaribu

Ziara ya kamati hiyo inaendelea mkoani Geita, kituo kinachofuata ni Chato.





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa