• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Maafisa Maendeleo ni Daraja la Kuwakwamua Wananchi Kiuchumi- Gombati

Posted on: November 19th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Ndugu Mohamed Gombati ametoa maelekezo kwa Maafisa Maendeleo ya jamii wanaofanya kazi katika Mkoa wa Geita kuhakikisha wanakuwa daraja litakalowavusha wananchi kiuchumi kutoka hatua moja hadi nyingine.

Ndg. Gombati ametoa kauli hiyo hivi karibuni alipokuwa akifungua rasmi kongamano la kwanza la Maafisa Maendeleo ya jamii Mkoa wa Geita lililofanyika katika ukumbi wa Nyerere uliopo kwenye viwanja vya Maonesho vya Dkt. Samia Suluhu Hassan Geita mjini hivi karibuni.

Katibu Tawala Mkoa wa Geita amefafanua kuwa moja ya jukumu la Maafisa Maendeleo ya jamii ni kutambua fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana katika maeneo yao zikiwemo za kilimo cha umwagiliaji, ufugaji, biashara ndogondogo na nyinginezo.

“Jamii yoyote iliyo bora inajengwa na Maafisa Maendeleo ya jamii hivyo hakikisheni fursa zote zilizoko katika maeneo yenu zinachangamkiwa na kutumiwa ipasavyo, ikiwemo fursa ya mikopo yenye riba nafuu inayotolewa na Serikali pamoja na taasisi nyingine za kifedha sambamba na ruzuku nyinginezo kama vile pembejeo za kilimo, mifugo nk.” Aliongeza Ndg. Gombati.

Afisa Maendeleo ya jamii Mkoa wa Geita Bi. Martha Kaloso ameeleza kuwa lengo kuu la kongamano hilo ni kujenga uelewa wa pamoja katika kusimamia taratibu kwa ajili ya kutekeleza shughuli za kujenga jamii kwa ufanisi mkubwa na anaamini kuwa kongamano hilo litaongeza uwajibikaji kwa jamii kupitia Maafisa Maendeleo ya jamii.

Akizungumza kwa niaba ya Maafisa Maendeleo ya jamii wenzake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamii kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale Bw. Majagi Maiga ametoa shukrani kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kutambua umuhimu wa Maafisa Maendeleo ya jamii wa Mkoa mzima kukutanishwa ili kujadili changamoto zinazowakabili katika maeneo yao, kubadilishana uzoefu wa kazi na kuweka mikakati ya namna ya kujikwamua kutoka katika changamoto zinazowakabili katika utendaji kazi wao wa kila siku.

Kwa upande wake mwezeshaji Carlos Gwamagobe kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum amewataka Maafisa Maendeleo ya jamii katika Mkoa wa Geita kuendelea kuwasaidia wananchi kuchangamkia fursa nyinginezo za kiuchumi na siyo kutegemea shughuli za uchimbaji madini pekee.

Kongamano la kwanza la Maafisa Maendeleo ya Jamii katika Mkoa wa Geita liliongozwa na Kauli Mbiu isemayo “ Uchechemuzi ni dira ya matokeo chanya kwa jamii” moja ya shughuli iliyofanyika ndani ya kongamano hilo ni  utoaji tuzo kwa Maafisa Maendeleo ya jamii waliofanya vizuri katika kuhamasisha wanufaika kurejesha mikopo inayotolewa na Serikali kwa vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalum ndani ya muda unaotakiwa ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Chato imeibuka kinara ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe na Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale imeshika nafasi ya tatu.


Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Ushirikiano wa Walimu na Wazazi Waongeza Ufaulu Nyang'hwale

    December 05, 2025
  • Ugonjwa wa Selimundu Kupatiwa Utambuzi Geita

    December 05, 2025
  • Serikali Kujenga Maabara ya Kisasa ya Uchunguzi Madini Geita

    December 02, 2025
  • Maafisa Maendeleo ni Daraja la Kuwakwamua Wananchi Kiuchumi- Gombati

    November 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

MAKALA YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI MKOANI GEITA.
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa

  • Situs Toto
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • YAMITOTO
  • Situs Toto
  • Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Togel
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • YAMITOTO
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • DORA77
  • Situs Toto
  • KOI200
  • Situs Toto
  • Toto Slot
  • Situs Toto
  • DORA77
  • Situs Toto
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200
  • AXL777
  • DORA77
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • AXL777
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • Situs Toto
  • KOI200
  • KOI200
  • YAMITOTO
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • Toto Slot Gacor
  • NABITOTO
  • AERO88 Slot Gacor