• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Maafisa Maendeleo ya Jamii Waaswa Kutunza Pikipiki

Posted on: October 24th, 2025


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na makundi maalum Bw. Amon Mpanju amewaasa Maafisa Maendeleo ya Jamii waliopatiwa pikipiki ambazo zimetolewa na Serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzitunza pikipiki hizo na kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa na sio shughuli zao binafsi.

Bw. Mpanju ametoa wito huo tarehe 24 Oktoba 2024 alipokuwa akikabidhi pikipiki nane kwa Maafisa Maendeleo ya jamii wa Kata za Muganza, Kigongo, Lwamgasa, Shabaka, Uyovu, Namonge, Masumbwe na Lulembela. Hafla fupi ya ugawaji wa pikipiki hizo umefanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii ameeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejikita katika kutekeleza matakwa ya kikatiba ya kugatua rasilimali fedha, ushushaji wa huduma Pamoja na watumishi ili kuwafikia wananchi wote walioko katika vitongoji, vijiji, mitaa na Kata na katika hili ndani ya miaka miwili Sekta ya Maendeleo ya Jamii imeajiri watumishi zaidi ya elfu moja.


“Serikali imeona kuajiri wataalam wa Maendeleo ya Jamii kwenye Kata pekee bila kuwapatia vitendea kazi inakuwa haitoshi kama tunavyojua jiografia ya Nchi yetu ni pana, kuna baadhi ya wananchi wanaishi mbali na Makao makuu ya Halmashauri. Hivyo Maafisa Maendeleo ya Jamii ambao ni wachechemzi na wahamasishaji wakubwa wa maendeleo ambao wanatakiwa wahakikishe wananchi wanatambua fursa mbalimbali zinatozolewa na Serikali ikiwemo mikopo yenye riba nafuu kwa kuwahamasisha katika maeneo yao.

Bw. Mpanju ameongeza kuwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Kata wana uwezo, mbinu na kuamsha ari ya maendeleo katika ngazi ya msingi kwa kutekeleza majukumu mbalimbali kwa manufaa ya jamii lakini wanahitaji nyenzo za kuwawezesha kuwafikia wananchi hao. Hivyo katika kutambua hilo Serikali imeweka utaratibu wa kununua pikipiki kila mwaka, ambapo katika mwaka wa fedha 2025/2026 imenunua pikipiki 98 kwa Nchi nzima ili kuboresha utendaji kazi wa Maafisa hao wakishirikiana na wataalam wengine kwenye Kata na kutimiza majukumu yao kiufanisi.

Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Geita Bi. Martha Kaloso ameeleza kuwa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Geita inakabiliwa na uhaba wa vyombo 131 vya usafiri kwa wataalam wake katika ngazi ya Kata hali inayopelekea uwajibikaji hafifu wa kuwafikia wananchi walioko maeneo ya vijiji vya mabli, ufuatiliaji hafifu wa shughuli za miradi ya maendeleo ya Jamii na ufuatiliaji hafifu wa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Ndg. Wajama Bwire, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Namonge Wilaya ya Bukombe ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwakumbuka na  kuwapatia pikipiki zitakazowawezesha kutoa huduma kwa wananchi katika maeneo ambayo yako mbali na makao makuu ya Halmashauri zao.





Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Maafisa Maendeleo ya Jamii Waaswa Kutunza Pikipiki

    October 24, 2025
  • Wananchi Geita Kupata Maji ya Uhakika Disemba 2025

    October 21, 2025
  • Visima 150 Kuwanufaisha Wakulima Mkoani Geita

    October 17, 2025
  • Wakandarasi wa Maji Watakiwa Kukamilisha kazi kwa Wakati

    October 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa