• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MAWAZIRI UGANDA WATEMBELEA MIGODI LWAMGASA NA NYARUGUSU GEITA

Posted on: November 29th, 2017

MAWAZIRI  UGANDA WAVUTIWA NA UCHIMBAJI MDOGO WA DHAHABU MKOANI GEITA

Mawaziri wa nne wa Wizara za Madini,  Uchumi, Mambo ya Ndani na Nje  wa Serikali ya Jamhuri ya Uganda wamewasili Mkoani Geita kujifunza namna Serikali ya Tanzania ilivyofanikiwa kuwezesha na kuendeleza Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu ili kukuza Sekta hiyo nchini kwao.

Akizungumza kwa niaba ya Mawaziri wengine baada ya kuwasili katika Mgodi wa Busolwa Mine Waziri wa Nchi na Maendeleo ya Madini wa Uganda Mheshimiwa Lokeris Peter amesema kuwa wamekuja Tanzania kujifunza mbinu za kuendeleza Sekta ya Madini hususan Uchimbaji Mdogo kwa kuwa Tanzania imekuwa ikifanya shughuli hii kwa muda mrefu na kupata  mafanikio makubwa. Mheshimiwa Peter ameongeza kuwa wamekuja Geita kwa kuwa ni kuna migodi mingi mikubwa na midogo hivyo wamekuja kujifunza namna wanavyochimba, kuuza, kuunganisha wachimbaji katika vikundi na namna wanavyothibiti utoroshaji wa madini ili nao wakawaendeleze wachimbaji wa dogo nchini Uganda kwa nia ya kupata maendeleo kama Tanzania.

Awali akizungumza katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Stanslaus Nyongo Naibu Waziri wa Madini amesema kuwa Tanzania tumepata maendeleo makubwa ya kuweza kuendeleza wachimbaji wadogo, kati na wakubwa hivyo Mawaziri wanne na Wanasheria kutoka Uganda wamekuja nchini  kuona ni jinsi gani Serikali ya Tanzania ilivyofanikiwa kuendeleza na kusaidia uchimbaji wa madini mdogo, kati na mkubwa. Amesema "wametembelea nchi nyingine za Afrika lakini bado wameona kuna umuhimu wa kufika Tanzania kwasababu kila nchi waliyofika waliona Tanzania ni mfano kwa Afrika hivyo wamekuja kujifunza na kuona namna nchi inavyoneemesha wananchi wake kupitia sekta ya madini baada ya mabadiliko ya sheria ya madini ya mwaka 2010 kwenda Sheria mpya ya mwaka 2017 na mabadiliko yake na sera za nchi kwa jumla ". Ameongeza kuwa wamekuja Geita kwasababu kuna madini na wachimbaji wadogo wengi zaidi ili waone jinsi wachimbaji wadogo wanavyowezeshwa kupata mitaji ya kufanya shughuli za uchimbaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameipongeza Serikali ya Uganda kwa kuona umuhimu wa kuja kujifunza Geita na kutambua jinsi Sekta ya madini inavyoweza kuleta mageuzi ya uchumi wa nchi. Ametoa wito kwa wachimbaji wadogo mkoani hapa kujiunga katika vikundi ili kuunganisha nguvu, mitaji na uzoefu wao kwa pamoja na walete vifaa vya kisasa na kuwa na uchimbaji wa kisasa wenye tija ili mitaji yao ipanuke  na kupata faida ili kuongeza ajira nyingi kwa watanzania.

Wakiwa Mkoani Geita Mwaziri hao pamoja na wataalamu wao wametembelea Wilaya ya Geita ambapo wamejionea shughuli za uchimbaji mdogo na kati katika migodi ya Busolwa mine uliopo kata ya Nyarugusu,Kadeo Mine na Kituo cha mfano cha Serikali kwa ajili ya kufundishia masuala ya uchimbaji wa madini kilichopo eneo la Lwamgasa Wilayani Geita.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa