• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Mgogoro wa Shambani Humalizwa Shambani”. Asema RC Shigela.

Posted on: December 29th, 2022

Na Boazi Mazigo-Geita

Ikiwa zimesalia siku kumi na mbili kufikia siku ya kupokea taarifa ya suluhu ya kudumu ya mgogoro uliodumu kwa muda mrefu baina ya Wananchi wilayani Geita na Mgodi wa Dhahabu Geita (GGML) kuhusu fidia kwenye eneo lenye leseni ya uchimbaji inayomilikiwa na mgodi huo, mkuu wa mkoa Geita mhe.Martine Shigela amefanya ziara na kujionea uhalisia mipaka iliyowekwa kwenye eneo llinalouzunguka mgodi huo na kuwaomba wananchi kuendelea kuwa na utulivu wakisubiri uamuzi wa serikali juu ya hatima yao.

Akiongea baada ya kutembelea maeneo kadha wa kadha yenye vigingi vya mipaka ya mgodi huo Desemba 28, 2022, RC Shigela amesema ameona ni vyema kutembelea maeneo hayo yenye mgogoro ili kumsaidia pamoja na viongozi wengine kufanya maamuzi sahihi pale hatua ya kufanya hivyo itakapofikiwa huku akiwaahidi wananchi kuwa serikali iliyopo madarakani inamaliza changamoto waliyonayo hivi karibuni.

“kwanza niwashukuru viongozi wote kuanzia serikali za Mitaa, wananchi pamoja na mgodi kwa kazi tuliyoifanya kwa kushirikiana. Ninaamini mgogoro wa shambani, humalizwa shambani na ndio maana nilionelea nifike kuona kwa macho ili hata tunapokuwa kwenye hatua za maamuzi ya kupata suluhu ya kudumu basi tufanye tukiwa tunayaelewa vyema maeneo haya” alisema RC Shigela.

Aidha mkuu wa mkoa huyo aliongeza kuwa, ziara hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi madhubuti wa Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan baada ya kikao na viongozi wa juu wa mgodi na kwamba imedhamiria kuumaliza kabisa mgogoro huo ndani ya kipindi kifupi ili kuwaondolea adha wananchi wa Geita ili waweze kujiletea maendeleo na kuwapongeza viongozi kuanzia mbunge, diwani hadi mwenyekiti wa mtaa kwa namna wanavyofuatilia utatuzi wa kero hiyo.

Kwa upande mwingine, mkurugenzi mtendaji wa mgodi huo Bw.Terry Strong amesema anaushukuru uongozi wa serikali kwa jitihada na amejifunza mengi na hasa kuhusu mgogoro huo na kwamba wanahidi suluhu itapatikana kwani kupitia changamoto ndipo huibuka namna ya kutatua.

Ziara hiyo imehusisha viongozi mbalimbali wa serikali, Chama Cha Mapinduzi, pamoja na wananchi ambapo maeneo mbalimbali yametembelewa ikiwemo eneo la Katoma, Magema, Katumaini, Nyamatagata, Mgusu, Nyakabale n.k




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa