• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MKURABITA Kuanzisha Kituo cha Urasimishaji na Uendelezaji Biashara Mjini Geita

Posted on: July 5th, 2019

Serikali ya Awamu ya Tano Kupitia Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji Geita ipo mbioni kuanzisha kituo kimoja cha uimarishaji na uendelezaji biashara (one stop business formalization and development centre) katika jengo la soko kuu la dhahabu geita ikiwa ni miongoni mwa jitihada za serikali katika kuweka mazingira mazuri ya biashara kwa kuruhusu uwekezaji mkubwa wa kibiashara Mjini Geita.

Hayo yameelezwa Julai 4, 2019 Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Bw.Deodatus Kayango, akimwakilisha mkuu wa mkoa wa geita alipokuwa akisoma hotuba ya kuahirisha mafunzo ya siku 4 kwa washiriki 614 (wafanyabiashara na wajasiriamali) yaliyoandaliwa na MKURABITA katika ukumbi wa kanisa la Katoriki Mjini geita.

Akiahirisha mafunzo hayo, Bw.Kayango amesema kuwa, anaamini mafunzo yaliyotolewa yamewajengea uwezo wa kufanya biashara washiriki hao katika mfumo rasmi kwani kurasimisha biashara kutakuza biashara zao na kutawapa fursa kufanya kazi na taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kwa utaratibu wa zabuni, hivyo waichangamkie fursa kwakuwa Geita ni mkoa wa kimkakati.

“tambueni kuwa, uanzishwaji wa soko la madini na maandalizi ya eneo la uwekezaji kwaajili ya maonyesho ya biashara pamoja na shughuli za uchimbaji wa dhahabu utafungua fursa mbalimbali za uwekezaji, hivyo mzichangamkie fursa hizo kwani sasa mnaweza kuzibaini. Nawasihi kuwa makini kuyafanyia kazi mliyoyapata ili muweze kuboresha kipato muboreshe na maisha yenu lakini kubwa zaidi, tusichakachue bidhaa zetu”, amesema Kayango


Akihitimisha, Bw. Kayango amewakumbusha kujifunza uzalendo kwa kutoa na kudai risiti wakati wa biashara na pia anaamini mafunzo kutoka kwa wawezeshaji yatakuwa na tija kwao, kisha kukabidhi vyeti kwa baadhi ya washiriki.

Naye mwakilishi wa mkurugenzi wa mji geita bw. Zengo Pole ambaye ni Afisa Maendeleo ya Vijana amesema anawashukuru wawezeshaji wote pamoja na wadau MKURABITA kwa kuichagua geita. Vilevile amesema, kama halmashauri wako tayari kuwapokea wadau wengine wowote wa maendeleo na kuwashika mkono wafanyabiashara ili kuwakuza na ndiyo maana wanatoa asilimia 10 ya wanawake, vijana na wenye ulemavu na kuwashauri waitumie elimu waliyonayo wakichukua mikopo kutoka halmashauri ili wajiendeleze.

Awali akisoma taarifa fupi ya utangulizi mbele ya mgeni rasmi, meneja urasimishaji biashara wa MKURABITA bw. Harvery Kombe amesema, mafunzo hayo yalilenga kuwafikia watu 1000 lakini wameweza kutoa kwa 617 pekee. Vilevile wawezeshaji wametoka MKURABITA, benki na NMB, CRDB, TCCIA, SIDO, GODTEC, NSSF, STAMICO na halmashauri.

Uwepo wa Kituo cha urasimishaji na uendelezaji biashara utahusisha kupata kitambulisho cha uraia kutoka NIDA, kusajili majina ya biashara (BRELA) kutoa leseni za biashara, namba za utambulisho wa mlipa kodi (TIN) kupitia TRA, huduma za kibenki kutoka CRDB na NMB, na TBS kupitia SIDO.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa