• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mradi wa Postikodi Kufikisha Barua, Vifurushi na Mizigo Nyumbani

Posted on: October 2nd, 2019

Katibu Tawala Mkoa wa Geita Denis Bandisa amemuomba Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kuifanya Geita kuwa ya kwanza kwenye matumizi ya mpango wa anwani za makazi na Postikodi, huduma itakayomwezesha mwananchi kupata barua, mizigo au kifurushi atakachotumiwa akiwa kwenye makazi yake kutoka sehemu nyingine.

Ametoa ombi hilo Oktoba 2, 2019 mbele ya Naibu Waziri Nditiye baada ya kuwasili mkoani geita kwa ziara ya kikazi akiwa ameambatana na wataalam wa wizara anayoisimamia, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) pamoja na wawakilishi wa Kampuni ya VODACOM huku akieleza baadhi ya changamoto za sekta ya mawasiliano kutokana na ukuaji wake ikiwemo ya matumizi mabaya ya mitandao.

Mhandisi Nditiye amesema, sekta ya mawasiliano inakuwa kwa kasi sana, na kwa mataifa mengine ndiyo hutegemewa kwa uinuaji wa uchumi na inahitajika sana na watu hivyo ni sekta mtambuka, jambo linaloifanya Wizara kwaniaba ya Serikali kuhakikisha inatoa kipaumbele kwenye sekta hii na kuifuatilia kwa karibu sana kisha kueleza lengo la ziara yake.

“lengo la kufanya ziara Geita kwanza ni kuangalia hali ya mawasiliano kwa ujumla, pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hii. Pili, kutokana na changamoto za mawasaliano, tumekuja kuelimisha juu ya usajili wa laini za simu kwa alama za vidole tukitambua kuwa, endapo ifikapo desemba 31, 2019 bado mtu hajasajili laini kwa alama za vidole, basi mawasilano kwake yatakoma, hatoweza kupokea simu na ujumbe wala kupokea mpaka pale atakapojisajili, hili litapunguza changamoto ya wizi wa mtandao. Mwisho, ni uhamasishaji wa mpango mkubwa wa anwani za makazi ili tuepuke mtu kwenda posta kufuata mzigo, barua au kifurushi bali kimkute nyumbani”, alisema Mhandisi Nditiye kisha kumkabidhi Katibu Tawala Mkoa vitabu vya Taarifa ya Utekelezaji wa Mradi wa Mawasiliano kuendelea na ziara yake kwenye wilaya ya Mbogwe.

Akiwa njiani kuelekea wilayani Mbogwe, Mhandisi Nditiye amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akiwa katika ukaguzi wa hatua za ujenzi katika mradi wa kuzalisha gesi itokanayo na taka za machinjio, mradi wa halmashauri ya mji geita unaotekelezwa kwa fedha za Benki ya dunia na kumweleza lengo la ziara yake kisha kundelea na ziara yake.

Imeelezwa kuwa, hadi sasa kata zote nchini zina postikodi na kwamba zoezi lililobaki ili kukamilisha hatua ya mwananchi kupokea mzigo akiwa kwenye makazi yake ni la kuzifikia halmashauri zote, kisha kutambua majina ya barabara na kuweka namba za nyumba ili sasa mwanachi aweze kufikiwa popote alipo kupitia utambuzi huo. Pia, zoezi hilo litarahisisha utendaji hata kwa jeshi la polisi kwa kujua ni wapi mwananchi Fulani anaishi, lakini vilevile itarahisisha kuwakamata waarifu kwakuwa tayari namba zao zitakuwa zimesajiliwa kwa alama za vidole.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa