• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Programu ya IMASA Kuwainua Wananchi Kiuchumi

Posted on: September 20th, 2024

Programu ya IMASA Kuwainua Wananchi Kiuchumi Geita

Uanzishwaji wa program ya Imarisha Uchumi na mama Samia (IMASA) katika Mkoa wa Geita kutawezesha Zaidi ya wananchi elfu 64 kuinuka kiuchumi kupitia shughuli mbalimbali za uzalishaji mali wanazozifanya.

Kauli hiyo imebainishwa na Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika masuala ya wanawake na makundi maalum Ndugu Sophia Mjema alipokuwa akizungumza na wanavikundi walioshiriki hafla fupi ya kutambulisha programu ya IMASA Mkoani Geita tarehe 20/9/2024 katika ukumbi wa GEDECO Geita mjini.

Ndg. Sophia Mjema ameeleza kuwa ndoto ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona kila mwananchi anaunganishwa katika mnyororo wa kukuza uchumi kupitia bidhaa wanazozalisha, hivyo amewaagiza wao kama wajumbe wanaozunguka Nchi nzima kwa lengo la kutembelea na kuzungumza na wanachama wa majukwaa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi sambamba na kukagua shughuli zinazofanywa na majukwaa hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali watanzania wakiwemo wananchi wa Mkoa wa Geita kupitia fursa za kiuchumi kama IMASA na kuahidi kushirikiana na viongozi wa majukwaa kubaini shughuli zote zinazofanywa na wanavikundi, changamoto zinazowakabili sambamba na kuibua fursa zilizopo katika jamii.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe.Louis Bura ametoa ushauri kutengenezwa kwa mfumo rasmi ambao utawawezesha wakulima, wafugaji na wajasiriamali wadogo kupata fursa ya kukopeshwa mikopo isiyo na riba ambayo itawainua na kufikia hatua ya kufanya shughuli zenye tija. Pia ameziomba taasisi za kifedha kurahisisha mchakato wa upatikanaji wa mikopo ili kuendana na msimu wa kila biashara, kilimo nk.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara , Mwenyekiti wa Chemba ya wafanyabiashara Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amemshukuru Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kila mwananchi anainuka kiuchumi kupitia fursa mbalimbali kama IMASA na  kutoa mikopo yenye riba nafuu

Mhandisi Robert Gabriel ameongeza kuwa wao kama wafanyabiashara watajitoa kwa hali na mali katika kushirikiana na viongozi wa majukwaa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi.


Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi. Beng’i Issa amesema kuwa changamoto zinazowakabili wafanyabiashara, wajasiriamali kwa sehemu kubwa ni kutorasimisha biashara zao na ukosefu wa mafunzo wa mifumo mbalimbali inayotumika katika uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Bi. Beng’i Issa ameeleza kuwa program ya IMASA itahusika na uwezeshaji wa wanawake, vijana na makundi maalum katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na ile ya Tanzania visiwani ambapo program hiyo itaendeshwa kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Julai 2024 hadi Juni 2025 na itahusisha wanufaika Zaidi ya elfu sitini.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara Wadogo Wahamasishwa Kujisajili

    May 15, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa