• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RAS Gombati Ana kwa Ana na Balozi Mwanri Kuhamasisha Kilimo Bora cha Pamba Mbogwe-Geita

Posted on: November 23rd, 2023

Na Boaz Mazigo, Geita RS

Katibu tawala mkoa wa Geita bw. Mohamed Gombati ameishukuru bodi ya pamba kupitia balozi wa pamba nchini Aggrey Mwanri kufuatia mafunzo aliyoyatoa kwa maafisa ugani na wakulima wa halmashauri ya wilaya ya mbogwe lengo ikiwa ni kuhamasisha uzalishaji bora wa zao la Pamba lenye kauli mbiu "pamba ni dhahabu nyeupe"

Shukrani hizo amezitoa Novemba 23, 2023 wakati akihitimisha mafunzo kwa makundi hayo na kusema ni vyema viongozi kuhamasisha uzalishaji wa zao hilo kwakuwa ni la biashara na soko lipo.

"nikushukuru sana balozi Mwanri na bodi ya pamba kwa ujumla kwa kufundisha wataalam na wakulima wetu mbinu bora za uzalishaji wa zao hili. Pamba ni zao la biashara, hivyo ni wajibu wetu kuongeza nguvu na uwezo wetu katika uzalishaji wake. Tujitahidi angalau ndani ya miaka miwili tulime kilo milioni 20 na kila mmoja wetu angalau awe na heka moja ili tuwe mabalozi wa mfano kwakuwa pamba inaongeza ajira na kuondoa umasikini", alisema bw.Gombati.


Aliongeza kuwa, Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan anawapenda sana wananchi na ndiyo maana mbolea hupatikana kwa bei ya ruzuku ya serikali, vinyunyizi na dawa hupatikana bure, hivyo ni vyema maafisa ugani kutumia fursa hiyo kuhamasisha wakulima na wananchi kwa ujumla kuzalisha kwa ubora na viwango.

Bw.Gombati alimaliza kwa kutoa wito kwa maafisa ugani kuwa, kwa namna kiongozi wa nchi alivyoweka mazingira wezeshi, watumishi wana wajibu wa kumlipa kwa kufanya kazi kwa bidii.

Kwa upande wake Balozi wa zao la Pamba nchini Aggrey Mwanri alimpongeza sana mhe.Rais Samia kwa utoaji wa dawa bure na mbolea ya ruzuku, na kwamba ameweka mazingira wezeshi ikiwa lengo ni kuzalisha Tani milioni 1 ifikapo mwaka 2025 na endapo lengo hilo litafikiwa, Tanzania itakua nchi ya kwanza barani Afrika.

Mafunzo hayo yalihitimishwa kwa kuambatana na kiapo walichoapa wakulima na maafisa ugani kuwa mafunzo waliyopewa watayatumia ipasavyo ili kuleta matokeo.

Hakika, Pamba ni Dhahabu Nyeupe.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa