• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Rc Gabriel Awatumia Salamu Wanaoendelea Kutorosha Carbon Geita

Posted on: July 11th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Gabriel ameendelea kutoa onyo kwa wote wanaoendelea kutorosha carbon zenye madini ya dhahabu na kuzipeleka nje ya Mkoa wa Geita. Ni baada ya kupokea taarifa ya Mapendekezo ya Jinsi ya Kuratibu na Kuthibiti Shughuli za Uchimbaji, Uchenjuaji na Biashara ya Madini ya Dhahabu Mkoa wa Geita kutoka kwenye Kamati aliyoiunda tarehe 12.04.2018 yenye wajumbe kumi na tano (15) kutoka mbalimbali kama TAKUKURU, Jeshi la Polisi Ofisi za Madini Mkoa, RS Geita n.k iliyomaliza muda wake tahere 22.06.2018

Awali Mhe. Mhandisi Gabriel alianza kwa kuipongeza kamati kwa kazi nzuri waliyoifanya akisema ana imani nayo na kupokea mapendekezo waliyoyatoa lengo ikiwa ni kuokoa mapato ya Serikali yaliyopotea kwa muda mrefu.

Miongoni mwa mambo ambayo kamati iliyoyabaini ni pamoja na wafanya biashara kusafirisha carbon nje ya Mkoa wa Geita kwa kutoa sababu kwamba Elution nyingi za Geita (majiko ya kuchomea dhahabu) hazina Maabara ambazo zingewasaidia wamiliki wa ‘carbon’ kutambua kiwango cha dhahabu (ppm au g/t) kilichomo ndani ya carbon, hivyo kuwa na uhakika juu ya kiwango cha dhahabu kitakachopatikana baada ya kufanyika uyeyushaji (smelting), jambo lililopelekea Mkuu wa Mkoa wa Geita kutolea ufafanuzi suala hilo akisema, “napenda kuwatoa hofu wafanya biashara wote wa dhahabu kuwa , kwa sasa Mkoa wa Geita una Elution zenye uwezo kwa kushugulikia jumla ya tani kumi (10) za Carbon kwa siku kwa Teknolojia ya kisasa ya High Pressure yenye uwezo wa kuchoma carbon kwa masaa ishirini na nne (24) na ya gharama nafuu tofauti na Teknolojia ya zamani ya Low Pressure inayotumia masaa 48-55 yenye gharama kubwa za uendeshaji na nyingine zinajengwa, lakini pia kamera za Usalama (CCTV) zimefungwa hivyo kumhakikishia usalama wa uzalishaji katika Elution hizo”. Pia alitoa onyo kwa wote wanaotorosha carbon kupitia magari na kuagiza kuwa, endapo watatokea watu wataokamatwa wakitorosha carbon, itumike Sheria ya Madini ya Tanzania, Sheria namba 14 ya Mwaka 2010 na Marekebisho yake ya Mwaka 2017 ambapo atakayekamatwa, atalipa faini isiyopungua Milioni Tano na Isiyozidi Milioni Kumi kwa mtu binafsi na Milioni Hamsini kwa kampuni pamoja na utaifishaji wa mali zao.

Mwisho, Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Bw. Mohamed A. Majaliwa na Katibu wake Bi. Asha Rajabu walimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwateua na kuiamini kamati yao hadi kupata taarifa itakayoweza kuusaidia Mkoa katika kupanga mikakati ya kuokoa mapato ya Serikali yaliyopotea muda mrefu.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa