• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Geita akabidhi zawadi kwa washindi, wateja wa Benki ya CRDB

Posted on: July 10th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, amekabidhi jumla ya Tv Screen tatu (3) na ving’amuzi vitatu (3)  kwa washindi ambao ni wateja wa Benki ya CRDB tawi la Geita katika kampeni inayoendeshwa na Benki hiyo katika msimu huu wa Kombe la Dunia iitwayo “Shiriki Kombe la Dunia FIFA 2018 na Tembocard Visa.

Baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi, Mhe. Mhandisi Gabriel alitoa pongezi kwa uongozi wa Benki hiyo kwa hamasa ambayo wamekuwa wakiitoa kwa wateja lakini pia kwa huduma muhimu kama hiyo ya malipo ya mtandao. Aliwashukuru kwa kuwahakikishia wateja usalama wa fedha zao kwani kwa kufanya hivyo wanalinda uhai wa wageni na wananchi wa Geita na kwa kuwa hawatakuwa wakitembea na fedha nyingi mifukoni.

Alisema “nawapongeza washindi wote, watumia huduma ya Malipo ya Mtandao lakini Meneja wa Benki hii na Wafanya kazi wenzake nawapongeza kwa kuwa mimi kama Mkuu wa Mkoa sijawahi kupokea malalamiko yoyote kutoka kwa wateja wenu juu ya huduma zenu ofisini kwangu, hivyo basi tabasamu wanaloingia nalo wateja kwenye Benki yenu hakikisheni linajizalisha mara mbili yake” kisha kukata keki pamoja na washindi.

Mhe. Mhandisi Gabriel, aliendelea kwa kutoa wito kwa taasisi mbalimbali zikiwemo za Afya pamoja na wananchi wa Geita kwa ujumla kujiunga na aina hiyo ya huduma kwani ni njia rahisi na salama, jambo linalothibitika kupitia taasisi chache zilizotajwa na Benki ya CRDB Geita kama watumiaji wa huduma hiyo.

Akitoa utangulizi wakati wa ufunguzi wa hafla hiyo fupi, Meneja wa Benki ya CRDB Tawi lilipo Mjini Geita Bw. Amini Mwakang’ata alisema, kampeni hiyo ilianza mwezi Aprili, 2018 na inatarajia kuhitimishwa Mwezi Julai, 2018 lengo ikiwa ni kuwahamasisha wateja wake kutumia huduma ya Malipo ya Kimtandao (Online Payments) kupitia Tembocard Visa inayomwezesha mteja kununua bidhaa hata kama hana fedha mfukoni, njia ambayo ni salama kwa mnunuaji na muuzaji. Aliendelea kwa kutaja taasisi ambazo tayari zimejiunga na huduma hiyo kuwa ni pamoja na RK Supermaket, Lenny Hotel pamoja na kituo cha mafuta kiitwacho Mwatulole Filling Station na kuwahimiza wale wote wanaosita kutumia huduma hizo basi wajiunge.

Bw. Mwakang’ata aliwataja washindi wa kampeni hiyo kuwa ni wananchi watatu wakazi wa Geita ambao ni ambao ni Bw. David Hugg, Meneja kampuni ya GPH ambaye pamoja na zawadi zilizotolewa ameshinda kwenda Nchini Urusi ambapo atashuhudia Nusu Fainali ya Kombe la Dunia, Mhandisi Jonas Maluku kutoka TANROADS Geita pamoja na Bw. Gerald Midenyo. Watumishi na washindi walimalizia kusherekea ushindi huo kwa burudani na kula keki iliyokuwa imeandaliwa.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa