• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Geita Aketi na Golden Ridge Kujua Sababu ya Anguko Lao Kielimu

Posted on: July 16th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amekutana na kufanya kikao na uongozi wa shule ya Sekondari ya binafsi (High School) Golden Ridge iliyoko Mjini Geita ili kujua ni kwanini wamekuwa miongoni mwa shule kumi za mwisho Kitaifa na kutia doa kwenye Mkoa ilihali Mkoa kwa sasa una jitihada za kuinua kiwango cha elimu na maisha ya wananchi kwa kuboresha miundombinu ya Elimu na Afya. Ni kufuatia taarifa ya matokeo ya kidato cha sita mwaka 2018 iliyotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).

Mhe. Mhandisi Gabriel amempa angalizo mkuu wa shule hiyo kwa kumshauri aepuke kupokea wanafunzi wa madarasa ya mtihani kama kidato cha nne na sita bila kuwapima na kujua uwezo wao, jambo ambalo lisipozingatiwa vizuri huleta athari kwenye matokeo ya mitihani hasa ya mwisho ya Kitaifa.

Amesema “mwalimu, nenda ukafanye mapinduzi kwenye shule yenu, zinatieni vigezo. Wafuatilieni wanafunzi wanaohamia shuleni kwenu, na  wale wa madarasa ya mitihihani mjiridhishe na walikotoka lakini pia kwakuwa shule yenu ni ya mchanganyiko, mjitahidi kufuatilia maadili ya wanafunzi ili kusitokee athari zozote za kimaadili na kinidhamu”. Pia Mkuu wa Mkoa aliwaagiza wataalam wa idara ya Elimu Halmashauri ya Mji Geita kushirikiana na wataalamu wa elimu Ofisi ya Mkoa kupitia wadhibiti ubora wafanye ukaguzi kujiridhisha na ubora wa elimu inayotolewa na waalimu wa shule hiyo.

Akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Shule hiyo Mwl. William Kachinde alieleza kuwa, amefanya jitihada kubwa ilhali ni mgeni shuleni hapo na miongoni mwa sababu kubwa iliyosababisha anguko hilo kitaaluma kwenye matokeo ya kidato cha sita, ni kupokea wanafunzi wahamiaji kumi na mbili (12) wanaofanya jumla ya wanafunzi kumi na nne (14) kupata ziro kwenye matokeo hayo wavulana wakiwa 10 na wasichana 2. Ili kuweka kumbukumbu sahihi, Mwl. Kachinde alieleza kuwa kwa mujibu wa matokeo hayo, shule hiyo imekuwa ya mia tatu thelathini na nne (534) kati ya shule mia tano arobaini na tatu (543) Kitaifa na kuingia katika orodha shule kumi za mwisho. Kisha alihaidi kufuata ushauri uliotolewa ili hali hiyo isijirudie kwa kuwa wao kama shule pia hawakupenda kuteleza kwenye matokeo hayo.

Naye Kaimu Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji Geita Mwl. Ramadhan Khalfan amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa, kwa upande wake ameona sababu nyingine ni kitendo cha mmiliki wa shule kuwa na tabia kubadili wakuu wa shule hiyo mara kwa mara na ndani ya kipindi kifupi, jambo ambalo kiutawala lina athari na kusema wamekuwa wakikaa na uongozi wa shule hiyo kwa mashauriano na atatekeleza yote waliyoelekezwa ili kuondoa tatizo hilo.

Matokeo ya Shule ya Sekondari Golden Ridge ni kama ifuatavyo; (Div I=3, Div II=31, Div III=79, Div IV=21 na F au 0 =14), katika Jumla ya wanafunzi 154 waliofanya mtihani. Waliofaulu ni wanafunzi 134, wastani wa GPA ya 4.0428, na imekuwa shule ya kumi (10) kati ya shule (10) ndani ya Mkoa wa Geita.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa