• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Geita Aongoza Wakazi wa Shilabela, Kampeni ya Usafi Mtaa kwa Mtaa, Akemea Waganga Wenye Ramli Chonganishi.

Posted on: November 4th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amezindua kampeni ya usafi wa mazingira ya mtaa kwa mtaa itakayodumu mwezi mzima ikihamasisha usafi kuwa endelevu katika kuhakikisha Mji wa Geita ambao umekuwa ndoto ya wana Geita kuwa Manispaa basi ufikie hatua hiyo kwa kuzingatia vigezo vyote ikiwemo usafi wa mji.

RC Gabriel amewaongoza wananchi wa Mtaa wa Shilabela, Kata ya Buhalahala kufanya usafi katika maeneo yote ya mtaa huo likiwemo eneo la soko tarehe 03.11.2018 ambapo mamia ya wakazi na wafanyabiashara wa eneo hilo wamejitokeza kuunga mkono juhudi za RC Gabriel akiwa mbele akiongoza zoezi hilo, huku akiwashukuru wananchi waliojitokeza wakiwa na vifaa mbalimbali vya usafi bega kwa bega pamoja naye.

Akiongea na wananchi baada ya zoezi hilo la usafi, RC Gabriel amesema, “tumezindua kampeni hii ya usafi, ni endelevu na ya mtaa kwa mtaa, tunajenga Geita mpya ili mji wetu ufanane na dhahabu kwakuwa wengine husema pamba ni dhahabu nyeupe, korosho ni dhahabu ya kijani ila Geita tunasema Dhahabu tunayo orijino yaani halisi” hivyo kuwahamasisha wananchi hao kuyatunza mazingira.

RC Gabriel ametoa onyo kwa watendaji wasiosimamia vyema matokeo ya fedha zinazochangishwa kwa wananchi kusafisha mazingira akisema ni lazima fedha inayokusanywa kwa ajili ya usafi zioneshe matokeo yaani maeneo yawe safi. Vilevile amekemea tabia ya baadhi ya watendaji kutokusoma taarifa za mapato na matumizi jambo ambalo huleta mashaka kwa wananchi. Wanaume pia wakaonywa kupitia hadhara hiyo kuhusu kuacha tabia za kuwanyanyasa kwa kuwapiga wake zao, huku waganga wa jadi wapiga ramli chonganishi wakifikishiwa ujumbe kuwa hawana nafasi Geita.

Hakuishia hapo tu, bali pia RC Gabriel ameitaka kampuni inayohusika na usafi Mjini Geita iitwayo Workers General Supply kuhakikisha maeneo yanakuwa safi na si kukusanya fedha pekee huku akiwaambia wananchi, “kama kuna mtu anataka kuhama Geita, mwambie ahairishe kwani yajayo si tu kufurahisha, bali yatashangaza”, huku akiwahakikishia usalama wa fedha za miradi ya jamii CSR zinazoendelea kuleta matokeo chanya ndani ya mwaka mmoja tangu kuteuliwa kwake.

Alihitimisha kwa kutoa namba yake ya simu akiwaambia wananchi waitumie kumwambia wanaowapa wanafunzi mimba, wazazi wanaowatumikisha watoto wa umri wa kwenda shule, watumia dawa za kulevya, vibaka na majambazi ili ashughulike nao akiwa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama.

Kwa upande wake Bw.Pancras Shwekelela, Afisa Mazingira kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mji Geita amewaambia wananchi kuwa, tayari yamefanyika mabadiliko ya sheria ya mazingira hivyo wajiandae kuipokea na kuitekeleza sheria hiyo mara itakapoanza kutumika kwa lengo la kuboresha usafi wa mazingira.

Mkurugenzi wa kampuni ya usafi Bw. Godwin Bagandanshwa na meneja wake Bw. Sixbert Tibaijuka wamemhaidi mkuu wa mkoa kufanya kazi kwa uaminifu huku wakiomba ushirikiano uendelee kutolewa na wananchi ili kurahisisha kazi wanayoifanya.

Awali Afisa Tarafa Geita Mjini Bw. Innocent Mabiki aliwashukuru wananchi kwa kuitikia wito huo na kuwaomba kulifanya zoezi hilo kuwa endelevu.





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa