• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RUWASA MBOGWE YAPONGEZWA KWA KUTUMIA MFUMO WA NEST

Posted on: October 2nd, 2024

RUWASA YAPONGEZWA KWA KUTUMIA MFUMO WA NEST

Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) wilaya ya Mbogwe imepongezwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 kwa kufuata taratibu za kutangaza zabuni za mradi wa maji katika Kata ya Ushirika Wilayani Mbogwe Mkoani Geita.


Akizungumza wakati wa uwekaji jiwe la msingi katika mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 Ndugu. Godfrey Eliakimu Mnzava amesema kuwa awali utaratibu uliokuwa unatumika kutangaza zabuni ulikuwa ni wa kubandika maombi na majibu ya waliopitishwa kutoa zabuni mbalimbali katika Taasisisi za Kiserikali, lakini Serikali ilibaini chembechembe za urasimu katika utaratibu huo.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ameongeza kuwa baada ya Serikali kubaini changamoto katika utaratibu wa awali wa utangazaji zabuni ilihamisha utaratibu wa manunuzi na zabuni kuhamia katika mfumo wa kidijitali ambao umeweka uwazi na uwajibikaji unaotembea na mapinduzi ya sayansi na Teknolojia kwa sababu vigezo vyote vimeainishwa na waombaji watatambua kama wana sifa za kupata zabuni au la. Hivyo viongozi wote wa Mkoa wa Geita wahakikishe Taasisi zote za umma zitumie mfumo wa NEST kwa masuala yote ya kutangaza zabuni za utekelezaji wa miradi na manunuzi mbalimbali.



Ndg. Godfrey Mnzava pia ametoa pongezi kwa klabu ya kupinga rushwa katika Shule ya Sekondari Mbogwe kwa kuelewa vyema tatizo la rushwa linavyoharibu utaratibu katika matukio mbalimbali kama uchaguzi, nafasi za kazi, vyuoni na maeneo mengine na kutoa elimu kwa wananchi kupitia vibonzo walivyochora ambavyo vimetoa taswira nzima ya tatizo la rushwa.


Mradi wa Maji safi na salama katika Kata ya Ushirika  ambao umegharimu Zaidi ya Shilingi Bilioni 2 utawanufaisha Zaidi ya wananchi elfu 20 wa vijiji vya Ushirika, Isebya, Ushetu, Mlale, Kadoke na Ikobe ambapo wananchi wa vijiji hivyo wametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za utekelezaji wa mradi huo ambao utakuwa msaada mkubwa sana katika utatuzi wa changamoto ya uhaba wa maji.


Ukiwa wilayani Mbogwe Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 umeweka mawe ya msingi, kuzindua, kukagua na kutembelea miradi tisa ya maendeleo ambayo imegharimu shilingi Bilioni nne.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa