• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Serikali Yatoa Zaidi ya Bilioni 40 Kujenga Miundombinu ya Umwagiliaji Geita& Mwanza

Posted on: August 12th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa shukrani kwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Tshs. Bilioni 40 kwa ajili ya kujenga na kukarabati miradi tisa ya umwagiliaji inayotarajia kuwanufaisha zaidi ya wakulima elfu 40 wa mikoa ya  Mwanza na Geita.

Mhe. Mtanda amebainisha hayo Agosti 08, 2025 alipokua akihutubia maelfu ya wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali katika kilele cha maadhimisho ya Nane nane Kanda ya ziwa magharibi yanayofanyika katika viwanja vya Nyamhongolo wilayani Ilemela mkoani Mwanza.

Pia ameeleza kuwa kwa kipindi cha 2020/25 serikali imetoa mbolea ya ruzuku ya Bilioni 6.4, Bilioni 4.7 kwa ajili ya ufugaji wa kisasa kwa vizimba ambapo zaidi ya vikundi 200 vimenufaika na Bilioni 263 zimetolewa kwa ajili ya chanjo za kuku na ng’ombe ndani ya mikoa hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ameziagiza Halmashauri kuendeleza viwanja hivyo kwa kuvijengea miundombinu ya kudumu na ya kisasa ili viwe na mazingira bora zaidi ya kuwahudumia wananchi katika kutoa elimu ya mashamba darasa kwa muda mrefu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uwekezaji mkubwa aliofanya kwenye sekta ya kilimo kwa kutuletea ruzuku ya pembejeo, kujenga maghala ya kutosha, kuwawezesha wavuvi kupata boti na nyavu pamoja na kuwapatia wafugaji madume yaliyoendelea kuboresha sekta ya mifugo.


Mhe. Shigela amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Maonesho ya Nanenane ambayo ni fursa kwa wakulima na wafugaji kama sehemu ya biashara, maarifa kujifunza ili wanaporudi katika shughuli zenu za kilimo, ufugaji na uvuvi  mkatumie maarifa mliyoyapata kuboresha na kuleta tija katika shughuli zao za uzalishaji.

Akitoa taarifa ya Maonesho hayo, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Bw. Peter Kasele amesema wadau wameongezeka kutoka 1110 (2024) hadi 1234 (2025) ikiwa ni ishara ya wananchi kuhamasika kutaka kujua matumizi ya teknolojia katika kuongeza uzalishaji.

Kilele cha Maonesho hayo kimehitimishwa na utoaji tuzo na zawadi ambapo Aqwa Eagle (Magu) wameongoza katika uvuvi wa samaki, Fredrick Katundala (Nyamagana) ufugaji Nyuki, Mkulima bora akiwa ni ndugu Bulimi Zakaria (Kwimba) na Shija Mashauri (Nyang’hwale) akiibuka mshindi katika ufugaji bora wa ng’ombe wa nyama.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Serikali Yatoa Zaidi ya Bilioni 40 Kujenga Miundombinu ya Umwagiliaji Geita& Mwanza

    August 12, 2025
  • UZINDUZI WA DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KATIKA MANISPAA YA GEITA

    August 07, 2025
  • DC Geita Azindua Rasmi Maonesho ya Nanenane 2025

    August 05, 2025
  • Bonana la Watumishi Linadumisha Afya ya Akili na Kujenga Ushirikiano- Gombati

    July 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa