• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Tani 50 za Alizeti Kuwanufaisha Wakulima Geita

Posted on: March 6th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela amepokea Tani 50 za mbegu ya alizeti kutoka Mamlaka ua Uthibiti wa Nafaka na mazao mchanganyiko ambazo zitagawiwa kwa wakulima katika Wilaya zote za Mkoa wa Geita.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya mbegu hizo hivi karibuni katika viwanja vya GEDECO Geita Mjini Mhe. Shigela amesema Serikali inabadili sura ya wananchi wa Mkoa wa Geita kuacha kutegemea uzalishaji wa madini pekee na kuanza kuamini kwamba kilimo kinalipa pia.

“Tunabadili sura ya wananchi wa Geita sio tu kutegemea katika uzalishaji wa madini lakini pia wanaojishughulisha na kilimo watambue kuwa Serikali inafanya jitihada ya kuwawezesha ili waweze kufikia malengo ya kujiondoa kwenye umaskini.”

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Geita, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba ameishukuru Serikali kwa kuwapatia wakulima tani 50 za mbegu ya alizeti kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Uthibiti wa nafaka na mazao mchanganyiko Bi. Irine Makota amesema Mamlaka imetoa mtaalam ambaye atakuwepo Mkoani Geita kwa ajili ya kutoa elimu ya upandaji mpaka mavuno kwa wakulima watakaopata mbegu hizo. Pia kutakuwa na mnunuzi ambaye ataingia mkataba na wakulima wote watakaopata mbegu hizo kwa lengo la kuhakikisha kunakuwa na soko la uhakika la zao la alizeti kwa wakulima.

Mmoja wa wakulima waliopokea mbegu za alizeti, Marseli Maliganya mkazi wa kijiji cha Nyamboge Kata ya Shiloleli ameishukuru Serikali kwa kutoa mbegu hizo ambazo zitachochea uzalishaji wa zao la alizeti katika Mkoa wa Geita.

Marseli amesema kuwa huu ni msimu wa tatu tangu aanze kulima zao la alizeti na ameona kuwa ni zao lenye tija na lina nafasi kubwa katika harakati za kuwainua wananchi kiuchumi endapo wataendelea kupatiwa ushirikiano kutoka Serikalini.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa