• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TARURA Chato Waendelea Kupasua Barabara Licha ya Changamoto ya Mvua

Posted on: April 1st, 2022

Licha ya kuwa na hali ya mvua inayoendelea maeneo mbalimbali mkoani Geita, Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini TARURA Wilaya ya Chato wamesema kuwa wakandarasi bado wapo kazini na wanaendelea na kazi, lengo ikiwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa wakati.

Hayo yameelezwa Aprili 1, 2022 na Meneja wa TARURA Wilaya ya Chato Mhandisi Daniel Mwiru wakati Timu ya wataalam kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita ilipofika wilayani humo kwa ajili ya kufuatilia miradi ya barabara inayotekelezwa na TARURA

Wakiongea wakati wa majumuisho baada ya kutembelea utekelezaji wa miradi, Timu ya Mkoa pamoja na TARURA Chato kwa pamoja wamesema, ni muhimu sana kutoa muda wa kutosha wa kumaliza kazi kwa mkandarasi kulingana na mazingira, ukitolewa mfano wa mvua zinazonyesha, maeneo yenye chemchem ambazo zimekuwa zikichelewesha miradi.

kwa upande mwingine,Bw. Last Lingson ambaye ni Afisa kutoka idara ya Mipango na Uratibu ambayo inahusika na Uratibu wa Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo pamoja na wataalam wengine (wakiwemo wahandisi) aliendelea kusisitiza kuwa ni muhimu sana kuhakikisha wakandarasi wanasimamiwa kwa ukaribu ili kuepusha kuchelewesha miradi lakini pia kuhakikisha kazi inayokamilika inakua haina mapungufu kwa ustawi wa Maendeleo ya taifa.

Hata hivyo, Mhandisi Mwiru aliongeza kuwa, usimamizi unafanyika kwa ukaribu kama ambavyo timu hiyo imeshuhudia kuwa kazi zinaendelea na mkandarasi yupo kazini lakini pia wao wamejipanga kulinda miundombinu kwanza kwa kutoa elimu kwa wananchi kupitia sheria zao, kisha kwa makubaliano wataweza kuitunza miundombinu. Vilevile, alisema kuwa, wao ni mashuhuda kwa jinsi fedha za tozo zilivyosaidia eneo kubwa

"tumejipanga na tayari tumekubaliana na wananchi kuwa, watakaa wenyewe na kukubaliana kutengeneza njia za kupitisha mifugo kwa miezi miwili na nusu kuanzia Aprili 1,2022 na kwa sehemu watakazohitaji kuvusha mifugo tutakubaliana tutaweka alama. Baada ya zoezi hilo, tutaanza kutumia sheria kutoa adhabu (faini) lengo kwa pamoja tuilinde miundombinu kwani zimetuia fedha nyingi kuijenga" alimaliza Mhandisi Mwiru.

Miradi ya Barabara iliyotembelewa ni pamoja na Matengenezo ya Muda Maalum Barabara ya Nyamirembe-Kazunguti ya urefu wa Km 2.2, Matengenezo ya Kawaida Barabara ya Nyabirezi-Kachwamba urefu wa Km 4.0, Matengenezo ya Muda Maalum Barabara ya Chabulongo-Nyang’homango urefu wa Km 3.3 zote za kiwango cha changarawe na katika hatua mbalimbali za matengenezo na Ujenzi wa Barabara ya Old CRDB kiwango cha Lami urefu wa Km 0.8 ambayo inaendelea kujengwa.

Geita ya Dhahabu, Utajiri na Heshima. Kazi Iendelee.

Boazi Mazigo

Afisa Habari

Geita RS



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa