• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TARURA Nyang’hwale Kuwaunganisha Mwingiro, Iyenze na Msalala (Kahama) kwa Milioni 119

Posted on: March 31st, 2022

Inakadiriwa kuwa zaidi ya wananchi wapatao elfu kumi (10,000) wanatarajiwa kunufaika baada ya ukamilishwaji wa Boksi kalvati (daraja) linaloendelea kujengwa kwenye Mto Iyenze katika mradi wa barabara ya Mwingiro-Ng’wasabuka katika Kata ya Mwingiro wilayani Nyang’hwale, daraja litakalowaunganisha wananchi wa vijiji vya kata ya Mwingiro ikiwemo vijiji vya Mwingiro, Iyenze na wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala iliyopo mkoani Shinyanga wilaya ya Kahama litakalogharimu kiasi cha Tshs.119, 000,000.

Hayo yameelezwa na wataalam wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini TARURA Wilaya ya Nyang’hwale Machi 30, 2022 wakati wa ziara ya timu ya wataalam kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita ambao wanaendelea kufanya ufuatiliaji wa miradi ya barabara inayotekelezwa na TARURA kwa mwaka wa fedha 2021/2022, ambapo kwa Nyang’hwale walipita kwenye miradi 6 yenye jumla ya Tshs. 545,731,000 zinazotokana na fedha za Tozo ya mafuta.

Akiongea akiwa kwenye maeneo mbalimbali ya miradi na wakati wa majumuisho, Bw.Last Lingson ambaye ni Afisa kutoka idara ya Mipango na Uratibu ambayo inahusika na uratibu wa ufuatiliaji na usimamizi wa miradi ya maendeleo akiwa na wataalam wengine wa ofisi ya mkuu wa mkoa aliwapongeza TARURA Nyang’hwale kwa namna wanavyoendelea kutekeleza majukumu yao kwenye usimamizi wa miradi mbalimbali ya barabara huku akiendelea kusisitiza juu ya usimamizi wa karibu zaidi kwa wakandarasi wanapoelekea kumaliza kazi, lengo likiwa ni kuleta matokeo kusudiwa.

“tuwapongeze TARURA Nyang’hwale kwa kuwa mmejenga barabara zenu vizuri, na mtakapokamilisha daraja lile kwenye Mto Iyenze na barabara ile ya Bukwimba-Bulangale kwa hakika mtakuwa mmewasaidia wananchi wengi kwani kwa kufungua barabara ambayo haikuwepo na kwa kuwaunganisha wananchi wa pande hizi za Mwingiro na Ng’wasabuka ni dhahiri mtachochea maendeleo kupitia sekta ya usafiri na usafirishaji” alisema Bw.Lingson.

Vilevile Bw.Lingson aliwakumbusha kuendelea kuhakikisha ushauri wote uliotolewa na wahandisi uzingatiwe ili kwa pamoja kufanikisha azma ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ya barabara.

Kwa upande wake Mhandisi Elson Moshi kutoka TARURA Nyang’hwale alisema, wao wamejipanga kuendelea kuwasimamia wakandarasi wote wanaotekeleza miradi kwenye wilaya yao na kuhakikisha wanatekeleza masharti ya mkataba lakini kubwa zaidi kutoa matokeo tarajiwa kwani japokuwa kazi hazijakamilika lakini tayari wanapata mrejesho kutoka kwa wananchi kuwa kazi wanayoifanya ni njema na inawasaidia wananchi, wakiahidi kuzingatia ushauri uliotolewa na wataalam ngazi ya mkoa. Mhandisi Moshi alieleza pia changamoto ya wakulima wanaolima karibu kabisa na miundombinu ya barabara pamoja na ile ya mifugo kupita kwenye barabara zilizotengenezwa ambazo hupekelea uharibifu mkubwa.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na matengenezo ya sehemu korofi katika barabara za Mang’ombe urefu wa Km.3.0, Nyashilanga-Nyamigogo urefu wa Km.3.0, Ujenzi wa Boksi Kalvati 1 katika barabara ya Mwingiro-Ng’wasabuka. Vilevile Matengenezo ya sehemu korofi katika barabara za Busolwa-Gamashi Km.11.4 na Nyamishishi-Shibalanga-Kaboha yenye urefu wa Km.7.0, na Ukarabati katiba barabara ya Bukwimba-Bulangale yenye urefu wa Km.5.0.

Pamoja na mvua zinazoendelea kunyesha, bado miundombinu hii inaendelea kustahimili na kuonekana iko vizuri na kwa hakika, kazi inaendelea.

Geita ya Dhahabu, Utajiri na Heshima. Kazi Iendelee

Boazi Mazigo,

Afisa Habari

Geita RS



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa