• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

"Tumedhamiria Kurudisha Uhai wa Mkoa Kupitia Uhifadhi”, asema Mhe.Senyamule

Posted on: February 12th, 2022

Mkuu wa mkoa wa Geita mhe.Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kuacha kuvamia misitu ili kulinda mazingira kwa maisha endelevu.

Mhe.Senyamule ameyasema hayo Februari 11 na 12,2022 alipofanya ziara kwenye hifadhi za misitu iliyopo wilayani Geita akiwa ameambatana na maofisa wa Wakala wa Misitu Tanzania TFS kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi juu ya uhifadhi wa mazingira, akipanda mti kwenye eneo la msitu wa Geita kama ishara ya uzinduzi wa kampeni ya uhifadhi wa mazingira  na kuwataka wananchi kuacha kuvamia na kujimilikisha maeneo ya hifadhi ili kuwa na jamii endelevu.

“tunamshukuru mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kata ya Lwamgasa nayo imepokea fedha za madarasa mengi kwenye mkoa pamoja na miradi mingine. Tumedhamiria kurudisha uhai wa mkoa kupitia uhifadhi, hivyo ni jukumu la kila mmoja kuwa mlinzi wa mwingine hasa baada ya mavuno ili baadaye tupande miti ili tutunze mazingira ikiwemo vyanzo vya maji. Vilevile niwahakikishie wananchi juu ya upatikanaji wa umeme kwenye vijiji 124 vilivyosalia kwani tayari serikali imetuletea mkandarasi mpya CSJE-CTCE Constrium kwaajili ya utekelezaji mradi wa REA III mzunguko wa pili kwa gharama ya Bilioni 25.4”, alisema mhe.Senyamule.


Wakati akimaliza kuongea na wananchi, mhe.Senyamule aliwakumbusha wananchi hao juu ya kujiandaa na sensa ya watu na makazi na kuwahimiza kushiriki na kutoa taarifa sahihi wakati zoezi litakapoanza.

Kwa upande wake Mhifadhi wa Misitu Wilaya ya Geita Almas Mggalu amesema, misitu ya Geita imeharibiwa kwa kiasi kikubwa na ndiyo maana wanakuja na mpango wa kuanzisha misitu ya kupanda kutokana na kuharibiwa ile ya asili na kuwataka wananchi kuendelea kuzingatia sheria iliyopo inayolinda hifadhi za misitu kwa manufaa yao ya sasa na ya baadae.

Aidha, wananchi wa Samina, Kata ya Mtakuja iliyopo halmashauri ya mji Geita na wa Lwamgasa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Geita wameendelea kuiomba serikali kuwapatia maeneo zaidi kwa ajili ya kilimo na ufugaji kufuatia maeneo yao kuzungukwa na mgodi pamoja na hifadhi za misitu ambapo awali mhe.Senyamule aliwaeleza kuwa, ni vyema kuendelea kusubiri tume iliyoundwa itakapoleta majibu juu ya maombi yao ya ardhi.


Katika ziara hiyo, mhe.Senyamule alisikiliza na kuelekeza utatuzi wa kero na changamoto mbalimbali zilizoibuliwa na wananchi wa maeneo hayo ili ziweze kushughulikiwa.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa