• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ukiuza Toa Risiti, Ukinunua Dai Risiti-Asisitiza RC Shigela

Posted on: August 12th, 2022

Na Boazi Mazigo- Geita

Hadi hivi leo Agosti 12, 2022 zikiwa zimebaki siku 11 kuelekea Sensa ya Watu na Makazi, Mkuu wa Mkoa Geita Mhe.Martin Shigela amefungua kikao kazi cha Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA cha kupitia malengo ya robo ya kwanza mwaka wa fedha 2022/23 kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Kagera, Geita, Mwanza, Simiyu na Mara katika Ukumbi wa Mikutano uliopo jengo la Otonde Mjini Geita msisitizo mkuu ukiwa ni kuhakikisha walipa kodi wanatoa risiti za mfumo EFD wanapouza huduma au bidhaa.

Akizungumza na washiriki wa kikao hicho ambao ni maafisa wa TRA, RC Shigela amewapongeza TRA Kanda ya Ziwa kwa kufikisha zaidi ya asilimia 100 ya lengo walilopangiwa na kutoa onyo kwa wafanyabiashara ambao wanashiriki kuipotezea serikali mapato kwa kutotoa risiti akisema ni kupitia kodi hizo wananchi ndipo hupata huduma za maji, elimu, afya, mishahara kwa watumishi n.k

Wakati huo huo, RC Shigela ametoa rai kwa wananchi kudai risiti wanaponunua bidhaa au huduma na kwamba hata ongezeko la mishahara na upandaji madaraja watumishi ni kunatokana na wananchi kuisaidia serikali kwenye eneo hilo kwani unapopewa risiti ya EFD ndipo serikali inapata mapato stahiki

"ninatambua kazi nzuri mnayoifanya TRA, nawaahidi ushirikiano kama kiongozi wa mkoa huu, na niwaombe tujipange kukusanya zaidi ya asilimia 100 ya lengo letu kwa mwaka huu, tutumie fursa aliyoitengeneza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwafanya Wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiari bila hata kutumia nguvu ambapo tumeshuhudia ndani ya mwaka mmoja wa Mhe.Rais, mapato yameongezeka kwa kiasi kikubwa". Amemaliza RC Shigela kisha kufungua kikao hicho cha siku mbili kuanzia Agosti 11-12, 2022.

Awali akisoma taarifa ya makusanyo ya kodi kwa mikoa hiyo ya kanda ya ziwa, Bw.Hashim Ngoda ambaye ni Meneja wa TRA Mkoa wa Geita amesema, kwa mwaka wa fedha 2022/23 hususan mwezi Julai, Mikoa ya Kanda ya Ziwa ilipangiwa kukusanya Bilioni 30.7 na kufanikiwa kukusanya zaidi ya Bilioni 35 sawa na asilimia 115, huku Geita pekee ikiongoza kwa kukusanya kwa asilimia 183.

Bw.Ngoda vilevile, amweleza RC Shigela juu ya changamoto zinazoikabili Geita zikiwemo Wafanyabiashara kutokutoa risiti za EFD, wananchi kutozidai risiti hizo, upitishwaji bidhaa kimagendo hali ambayo hupelekea kupoteza mapato ya ushuru wa forodha hali ambayo husababisha ushindani usio na uwiano sahihi lakini pia kuomba kusaidiwa na maafisa masuhuli kukusanya kodi ya zuio wanapofanya kazi na Wafanyabiashara, mambo ambayo RC Shigela ameahidi kuwekea msisitizo kama ambavyo ameombwa na TRA.

Naye Katibu Tawala Mkoa Geita Prof.Godius Kahyarara ametumia nafasi hiyo kujitambulisha kwa watendaji hao ikiwa ni mwendelezo wa kujitambulisha kwa watendakazi mkoani Geita na kisha kuipongeza TRA Geita kwa kuongoza kwenye kanda kwa mwezi Julai kwa kukusanya asilimia 183 ya lengo.

Jiandae Kuhesabiwa.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa