• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ushirikiano Baina ya Wataalam wa Elimu, Afya na Maji Watajwa Mwarobaini Kampeni ya Usafi na Mazingira, Mkoa wa Geita.

Posted on: January 10th, 2019

Ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazokwamisha Kampeni ya Usafi wa Mazingira Mkoani Geita, kimeendeshwa kikao cha kubadilishana uzoefu wa utekelezaji wa kampeni hiyo baina ya wataalam wa Kamati za Elimu, Afya na Maji na wadau (WEDECO) kutoka Halmashauri 6 za Mkoa wa Geita, kikao kilichofanyika tarehe 09.01.2019 katika Ukumbi wa Mikutano, Hospitali ya Wilaya Bukombe chini ya uratibu wa Bw.Elisante Shumbi, Afisa Afya wa Mkoa wa Geita.

Akisoma hotuba ya ufunguzi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Immaculata Raphael amewashukuru wajumbe kwa kuhudhuria, huku akiwataka kuwa na ushirikiano wakati wa kutekeleza kampeni hiyo, ambapo katika taarifa ya mkoa imeonesha kuwa bado utekelezaji si wa kuridhisha kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo uhamasishaji wa matumizi ya choo bora, uundwaji wa kamati za usafi na mazingira shuleni, upatikanaji wa miundombinu ya Usafi katika shule hasa za msingi n.k  

Amesema ,“ ni wakati sasa wa kuhakikisha mnafanya kazi kwa kushirikiana, vyoo vijngwe palipo na mtandao wa maji ili dhana ya vyoo bora ionekane, na ni kwa kushirikiana ndipo mtaalam wa elimu, maji na afya wataweza kufanikisha suala hili. Lakini pia ni muhimu kuunda klabu za kutosha mashulrni ili kampeni hii itekelezwe mashuleni kwa usahihi”

Pia, Mhandisi Raphael anatoa wito kwa kamati kufanya ukaguzi wa kiafya katika kambi mbalimbali za machimbo ya madini zinazoibuka kila wakati kwa lengo la kuthibiti uchafuzi wa mazingira kwa kuhakikisha kunakuwepo vyoo na miundombinu ya usafi, lakini pia usalama mahala pa kazi unazingatiwa na kuwahimiza watumishi kuendelea kuheshimu maelekezo yanayotolewa wakati fedha zinapoletwa ili kufanya kazi kusudiwa.

Wajumbe walipatiwa pia elimu juu ya usalama wa chakula na uthibiti wa magonjwa ya kuambukiza kutoka kwa Afisa ayfa na Mratibu wa Magonjwa ya Kuambukiza Mkoa wa Geita Bw. Jimmy Mtabwa, elimu iliyokumbusha juu ya kutotumia vyakula vilivyomaliza muda wake (expired), kupenda kupika chakula kitakachoisha siku moja yani kutopenda kula viporo na bila kuvipasha n.k

Mwakilishi wa WEDECO  Bw. Gwamaka Mwasandende, kwa upande wake alipendekeza kuwa, ni vyema wadau kuwa wanaendelea na mradi pale aliyetangulia atakapokuwa ameishia kuliko kila mdau anakuja na kuanza upya, jambo linalopelekea kurudi nyuma katika utekelezaji

Mwisho, wajumbe waliweza kujadiliana masuala kadha wa kadha na kuahidi kukamilisha yale yote waliyojipangia ikiwemo utengaji wa maeneo ya kuhifadhia taka, lakini pia kushindanisha vijiji katika upatikanaji wa kaya zenye choo bora kwa lengo la kuhamasisha usafi wa mazingira, ikiwa kubwa zaidi kuwa na ushirikiano wakati wa utekelezaji, kufanya kazi kama timu moja.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa