• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Vijana Wakumbushwa Kuchangamkia Mikopo ya Halmashauri

Posted on: September 3rd, 2025


Makundi maalum ambayo yanajumuisha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wamekumbushwa kuunda vikundi vitakavyowawezesha kupatiwa mitaji kutoka kwenye fedha za asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri zinazotolewa ili kuwakwamua watu hao kiuchumi.

Wasia huo umetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2025 Ndg. Ismail Ali Ussi alipokuwa akizungumza na vijana pamoja na wananchi wengine waliojitokeza katika Mbio za Mwenge wa Uhuru ulipotembelea kikundi cha vijana wataalam wa ufanisi katika Kijiji cha Ibambila Kata ya Nyang’hwale tarehe 03 Septemba 2025.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita imeondosha changamoto ya vijana kulalamika kukosa mitaji kwa kutoa fursa ya mikopo ya asilimia 10% hivyo ni jukumu la vijana kujiunda katika umoja utakaowawezesha kupata mitaji ya kuendesha shughuli mbalimbali za kiuchumi kutoka Halmashauri.


“ Vijana achene kulalamika kutokana na ukosefu wa ajira na ukosefu wa mitaji na badala yake mnatakiwa kubuni mbinu mpya za utafutaji wakati Serikali ikiwashika mkono kwa kutoa mikopo nafuu kwa ajili ya kuendeleza na kukuza mitaji yao.” Aliongeza Ndg. Ismail Ali Ussi.

Akieleza faida za mradi huo Katibu wa Kikundi cha vijana wataalam wa ufanisi amesema kuwa mradi huo umeweza kukuza uchumi kwa wanakikundi na kuongeza kipato cha familia zao, kutoa ajira kwa watu wengine wakiwemo mama lishe, wauza mbao na vijana wa ulinzi, kutoa mafunzo kwa vijana wengine juu ya ufundi pamoja na kufanya kazi na taasisi za Serikali ikiwemo Halmashauri kupitia kazi zinazotangazwa kwenye mfumo wa NEST.

Mwenge wa Uhuru 2025 umebeba kauli mbiu isemayo” Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu”. Aidha pamoja na ujumbe huo Mbio za Mwenge wa Uhuru unahamasisha wananchi kupambana na rushwa, kuzuia ugonjwa wa Malaria, mapambano dhidi ya UKIMWI na matumizi ya Dawa za kulevya na kuwaelimisha wananchi juu ya kuzingatia lishe bora.

Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Geita Wahamasishwa Kutumia Nishati Mbadala

    September 07, 2025
  • TFS Wapongezwa na Mwenge wa Uhuru 2025

    September 06, 2025
  • Vijana Wakumbushwa Kuchangamkia Mikopo ya Halmashauri

    September 03, 2025
  • Wawekezaji Wahamasishwa Kuwekeza Miradi ya Kijamii

    September 04, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa