• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Vijiji 12 Kuwashiwa Nishati Umeme Geita, Gereza la Butundwe Likiwemo

Posted on: February 19th, 2019

Tarehe 19.02.2019, wakazi na wananchi wa Mkoa wa Geita wameendelea kuhakikishiwa usambaziwaji na uwashiwaji wa umeme kupitia Mradi wa Umeme Vijijini REA, wakati wa ziara ya siku mbili mkoani hapa ya Waziri wa Nishati Mhe.Dkt.Medard Kalemani (Mb).


Hayo yamedhihirika baada ya Mhe. Dkt. Kalemani kuwasili Mkoani Geita akieleza lengo mahsusi la ziara yake, alipokutana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Gabriel ofisini kwake na kutoa pongezi za utendaji kazi kwa Mkoa wa Geita kwa kazi nzuri inayoendelea kufanyika na kumuomba kutosita kuwasilisha changamoto za nishati umeme kwa kadri zitakavyojitokeza.

Amesema, “kwanza nifikishe salamu za Mhe. Rais Magufuli kwa wanageita, anawasalimu sana na anawapongeza Geita mnafanya kazi. Nimekuja na wenzangu kufuatilia utekelezaji wa miradi ya REA, ambapo kwa sasa tupo katika hatua ya katikati ya utekelezaji huo ikiwa ni miezi 5 tangu Septemba 2018 kwa mkataba wa miezi 24, lakini pia kufuatilia hali ya kiumeme ndani ya Mkoa wa Geita na tunatambua bado haujaimarika kiasi cha kutosha, changamoto tunaendelea kuzipunguza lengo zitatuliwe na wananchi wanufaike na huduma ya umeme”.

Ameendelea kusema kuwa, kwa siku mbili (2) akiwa Geita, vijiji kumi na mbili (12) vitawashiwa umeme ambapo kwa Wilaya Geita kutakua na vijiji vine (4) likiwemo Gereza la Butundwe, ambalo kwa muda mrefu limekuwa gizani, hivyo watanzania walio gerezani watafurahia umeme kuanzia leo.

Mhe.Dkt. Kalemani amemhakikishia Mkuu wa Mkoa juu ya ufikishaji wa umeme kwenye nyumba za watumishi na majengo ya ofisi za serikali zilizopo eneo la Magogo, lakini pia  umeme utaendelea kufikishwa kwenye maeneo yote yenye uzalishaji wa dhahabu ili wananchi waweze kuchangia pato la taifa huku shirika nalo likipata faida.

kwa wale wote waliorukwa na umeme wa REA kwa namna moja ama nyingine, wameahidiwa kuangaliwa kwa utaratibu mwingine ili nao waweze kupata huduma hiyo muhimu, hivyo ameendelea kuomba ushirikiano kutoka kwa wananchi

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel alimkaribisha Mhe. Dkt. Kalemani akimuomba kufikisha salamu kwa Mhe. Rais Magufuli na kupongeza utendaji wa Wizara ya Nishati wa kasi katika kuhakikisha Tanzania ya Viwanda haikwami, lakini pia wananchi wanapata umeme, kisha kuomba umeme ufikishwe kwenye eneo la Magogo zilipojengwa nyumba za watumishi, hospitali pamoja majengo ya ofisi za serikali ikiwemo jengo la utawala Halmashauri ya Mji Geita.

Mradi wa REA awamu ya Kwanza unatarajiwa kukamilia ifikapo Juni, 2019 na kwa Mkoa wa Geita wenye vijiji 210, vijiji 45 kwa miezi mitano ndivyo tayari umeme umekisha washwa na 12 vitakavyowashwa leo vitafikisha  jumla ya vijiji 57,  na kwamba bado lengo ni kumaliza changamoto zote za nishati umeme. Kwa Nchi nzima vijiji 62 vinatarajiwa kuwashiwa umeme leo.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa