• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

VSO na SIDO Geita Wawawezesha Wajasiriamali 35 Kujikwamua Kiuchumi

Posted on: February 24th, 2022

Shirika lisilo la Kiserikali la VSO Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Mkoa wa Geita SIDO wamewazesha jumla ya vijana wajasiriamali 35 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 vifaa mbalimbali ili waweze kujikwamua kiuchumi baada ya kuwapa mafunzo ya wajasiriamali.

Hafla hiyo imefanyika Februari 24, 2022 katika ukumbi wa zamani wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka VSO, SIDO, Geita RS, Benki ya NMB Halmashauri za Geita na vikundi vya sanaa na burudani.

Akiongea kabla ya kukabidhi vifaa hivyo, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw.Musa Chogero ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita amewapongeza wote walioshirikiana kwa kuiunga mkono serikali kulisaidia kundi hilo la vijana kwani kwa kufanya hivyo ni kuongeza wigo wa kujitegemea katika uzalishaji na hivyo kuisaidia nchi kukua kiuchumi huku akiwataka vijana hao kuepuka tamaa ya fedha ili kuzingatia maadili na ubora wa bidhaa.

“niwapongeze VSO, SIDO, Halmashauri za Geita na wadau wote zikiwemo taasisi za kifedha kwa kuwasaidia vijana hawa kwani kwa kufanya hivi kuunga mkono juhudi za serikali kama ambavyo nayo hutoa 10% ya mapato ya ndani ya halmashauri kuwezesha makundi ya vijana, wanawake na wenye ulemavu, kwetu ni faraja kuona wajasiriamali hawa wanaongezeka. Siwezi kuacha kuwapongeza pia vijana kwa bidhaa nzuri zinazovutia, hongereni sana maana nimepita nimeziona bidhaa zenu”. Alisema Bw.Chogero


Katibu Tawala Huyo aliongeza kuwa, “ni vyema VSO mtufikshie shukran za dhati kwa wafadhili kutoka nchi ya Uholanzi na kwa hakika niwakumbushe wote tukumbuke kutunza mazingira yetu katika shughuli zetu kama ambavyo tumeelezwa juu ya kundi lililowezeshwa kutengeneza mkaa mbadala”. Alimaliza kwa kuwasihi taasisi za kifedha kubuni masharti nafuu ili kuwawezesha wajasiriamali hao kukopa kwenye benki hizo za NMB na NBC kisha kuzindua shughuli hiyo kwa kukata utepe na kugawa vifaa hivyo vilivyotolewa bure kwa wajasiriamali hao.

Wakitoa maelezo ya mradi, Meneja Mradi wa Clarity Bw. Elvis Chuwa na Mwakilishi wa Meneja wa SIDO Geita Bw.Bakari Kitobori  wamesema, mafunzo hayo yalitolewa kwa vijana 35 ambapo 8 walipewa mafunzo ya ushonaji nguo, 8 walipewa mafunzo ya utengenezaji wa sabuni na batiki, 8 walipewa mafunzo ya usindikaji wa vyakula mbalimbali na 8 walipewa mafunzo ya ufugaji wa kuku,  utengenezaji chakula cha mifugo na 3 walipewa mafunzo ya utengenezaji mkaa mbadala.

Viongozi hao wawili walieleza kuwa, mafunzo hayo yalichaguliwa na vijana wenyewe na hivyo wanaamini kupitia wao,vitazalishwa viwanda vidogo vingine vingi na wanaamini vijana hao wataongeza masoko kutokana na elimu waliyoipata.

Kabla ya kuanza kwa shughuli hiyo, mgeni rasmi alipita na kupewa maelezo juu ya bidhaa zilizotengenezwa na vijana hao baada ya kuwezeshwa mafunzo ya ujasiriamali kutoka SIDO kwa uwezeshwaji wa VSO



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa