• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI WATAKIWA KUSITISHA AJIRA ZA WATOTO GEITA

Posted on: June 16th, 2017

WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI WATAKIWA KUSITISHA AJIRA ZA WATOTO

Wachimbaji wadogo wa madini Mkoani Geita wametakiwa kuacha mara moja tabia ya kuajiri watoto wadogo kushiriki katika migodi midogo midogo iliyopo mkoani hapa kwa kuwa watoto hao wanatakiwa kuwa shule.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya wachimbaji wadogo wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa amewataka wachimbaji hao kuhakikisha hawatoi ajira kwa watoto wadogo katika maeneo yao ya migodi kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha maisha  na kuwanyima fursa ya kupata elimu. “kumekuwa na tabia ya kuajiri watoto wadogo katika maeneo mengi ya migodi tambueni kuwa watoto hao wanakosa masomo na pia mnahatarisha afya zao, hatua kali zitachukuliwa kwa mtu yeyote atakaye ajiri watoto katika mgodi wake’’.

Aidha, amewataka wachimbaji hao kuhakikisha wanakuwa na mpango mzuri wa kutunza mazingira katika maeneo ya shughuli za uchimbaji wa madini ili kuhifadhi mazingira ili baadae wakati wa ukomo wa mgodi mazingira yabaki katika hali nzuri.  Amewasisitiza wachimbaji wadogo kutumia elimu waliyoipata kuwaelimisha wachimbaji wengine ili kuboresha shughuli za uchimbaji wa madini ili kuweka hali nzuri ya usalama katika migodi kwa kuwa siku za hivi karibuni migodi imekuwa ikiporomoka mara kwa mara. Ameongeza kuwa kazi ya serikali ni kusimamia na kutoa elimu ili uchimbaji uwe katika hali nzuri hivyo wazingatia mafunzo hayo wakati wa utekeezaji wa shughuli zao za uchimbaji wa dhahabu. Vile vile amesema kuwa wakati umefika kwa Mkoa wa Geita kuwa na maduka ya vifaa vya uchimbaji wa madini pamoja na maduka ya Dhahabu kwa kuwa hakuna Mkoa hapa nchini wenye madini mengi ya Dhahabu kama ilivyo Geita hivyo, amewataka STAMICO na Kamishina wa madini kufuatilia ili huduma hizi muhimu zipatikane mkoani Geita.

Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya madini Mkoa wa Geita na kufadhiliwa na shirika la Plan International wachimbaji wadogo wameishukuru serikali na wadau hao kutoa mafunzo hayo ambayo kwao yana manufaa makubwa na watayatumia kuboresha shughuli za uchimbaji ulio salama na unaozingatia sharia na utunzaji wa mazingira.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa