• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wafanya Biashara Njooni; Elution Plant na Umeme Siyo Tatizo Mkoani Geita

Posted on: July 17th, 2018

Ni kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel alipofanya ziara ya kushtukiza na kujionea uzalishaji wa dhahabu katika Elution Plant (viwanda vya kuchomea Carbon zenye Dhahabu) mjini Geita.

Mhe. Mhanidisi Gabriel amefurahishwa na muitikio wa wamiliki wa elution plant hizo kuongezeka siku hadi siku ambapo ametembelea eneo la Nyanza lililoko Mbugani Mjini Geita lenye viwanda hivyo saba na kujifunza mengi ikiwemo jinsi dhahabu hiyo inavyopatikana.

Mkuu wa Mkoa ameshuhudia dhahabu yenye uzito wa Kilogramu moja na gramu mia mbili (Kg. 1.2) yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni Mia Moja (Tshs.100, 000,000/=) ndani ya dakika arobaini na tano (45) alizofika kwenye Elution Plant moja ya Mwananyanzala, hali iliyompelekea kusema;

“ninadhani mmeona wenyewe, carbon za kilo mia nne mteja wa kwanza, mia nne mteja wa pili tumepata kiasi hiki cha dhahabu, hii ni dalili njema kwa Mkoa na hizi ni kutoka Elution moja tena kwa dakika hizo, sasa vipi kwa Elution nyingine?. Ninataka fedha inayopatikana kwenye dhahabu irudi kwa jamii, ijenge miundombinu lakini pia wafanya biashara wa Dhahabu njooni tuna Elution saba hapa Nyanza eneo la Mbugani, hazina mzigo zinawasubiri mlete carbon lakini pia Kamera za usalama zipo (CCTV Camera), hakuna haja ya kuogopa na Mkoa uko shwari hakuna tatizo, Elution nyingine zinaendelea kujengwa ,gesi na transfoma za kutosheleza mahitaji yenu tumekwishazipokea shaka ondoa sasa” alisisitiza.

Moja ya wateja kutoka Nyarugusu Wilayani Geita (jina limehifadhiwa), alishukuru kwa namna ambavyo serikali inavyohusika kuanzia hatua ya kwanza anaweka mzigo wake hadi hatua ya upimaji kwani kwa kufanya hivyo hata yeye anaona hakuna nafasi ambayo ataibiwa mzigo wake na kumpongeza Mkuu wa Mkoa na Serikali kwa ujumla kwa jitihada anazoendela kuzifanya pamoja na wasaidizi wake kwa kuwa yeye kama mteja na Serikali ndiyo huweka makufuli kwenye mitambo ya kuchomea dhahabu hivyo hana hofu ya kuibiwa kama zamani.

Kwa upande wake moja ya wamiliki wa kiwanda cha Jema Africa, Elution Plant iliyokuwa ikifanya shughuli zake Mkoani Mwanza amesema, “kwakweli ninaziona faida za kuja Geita, wateja ni wengi, tofauti na nilivyokuwa kule, hivyobasi nawaita wateja waje tu ulinzi upo, Geita ni amani kazi zinaendelea”.

Kuelekea Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita, watanzania na wageni mnaalikwa kushiriki jukwaa hilo litakalofanyika kuanzia tahere 15-16.08.2018 linaloratibiwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) kwa kushirikiana na MKoa wa Geita ambapo mtaweza kushuhudia bidhaa zinazozalishwa Mkoani Geita lakini pia Maonesho Makubwa ya Teknolojia ya Dhahabu yatakayofanyika kuanzia tarehe 24-29 Mwezi Septemba, 2018.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa