• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

"Walimu na CWT, Tuisaidie Jamii Ijue Tulipotoka, Tulipo na Tunapokwenda" RC Geita Anena Hayo

Posted on: October 17th, 2020

Walimu na viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kanda ya ziwa wamekumbushwa juu ya wajibu walionao wa kuielimisha jamii juu ya wapi nchi ya Tanzania imetoka, ilipo na inapokwenda ili kuwa na  taifa la wazalendo wanaoipenda nchi yao na kwamba, watambue kihistoria mwalimu ni mkombozi wa taifa hili kupitia Hayati Mwl.Julius Nyerere.

Hayo yalielezwa ijumaa ya Agosti 16, 2020 na mkuu wa mkoa wa geita mhandisi Robert Gabriel alipokuwa akifungua warsha ya makatibu na makatibu muhtasi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wa mikoa ya kanda ya ziwa ya Mara, Mwanza, Geita na Kagera iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa JJ Hotel uliyopo Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro wilayani Geita.

Alisema, "msijidharau, ninyi ni wa pekee kwani hata ukombozi wa taifa hili uliletwa na mwalimu, hivyo ni imani yangu kwenu kuwa mnao wajibu wa kuieleza jamii tulipotoka, tulipo na tunapoelekea kwani kwa kufanya hivyo tutalisaidia sana taifa hili kuwa la wazalendo na wenye mshikamano kama ilivyo kaulimbiu yenu" kisha kuwaombea mafanikio akijipambanua zaidi kama shemasi wa mkoa.

Aliongeza kuwa, mwalimu ni kioo cha jamii, kioo cha taifa, mtu ambaye kazi yake hudumu milele na kwamba walimu wanapaswa kuyaenzi yale mema na misingi aliyoiacha baba wa taifa kwani misingi inapokuwa imara, maisha ya mtanzania huboreka na ndiyo maana hata kwa juhudi za kiongozi wa nchi yetu wa sasa ambaye pia ni mwalimu, amepambana na kutuvusha kwenye janga la korona kwa kumuomba Mungu lakini pia kutuvusha na kuingia uchumi wa kati .

kipekee mhandisi Gabriel aliwaeleza viongozi na watendaji hao kuwa, ndani ya kipindi kifupi Geita itakuwa ni mji wa kipekee, ikiwa kwa mwezi wa septemba, 2020 soko kuu la dhahabu lililopo mjini Geita liliendesha biashara ya Bilioni mbili kwa mwezi, huku ujenzi wa soko jingine la kisasa ukiendelea katika mamlaka ya mji mdogo katoro na kuwaeleza kuwa kila wilaya imepangwa kuwa na soko zuri la kisasa la biashara hivyo kuendelea kuwakaribisha wananchi wote kuwekeza mkoani hapa.

Akitoa neno la shukrani, katibu wa CWT mkoa wa Mwanza mwl. Daniel Mafwili alimshukuru na kumwomba mkuu wa mkoa kufikisha salamu zao kwa mhe.Rais Magufuli kwani amekuwa msikivu sana kwao na kwamba wanamuombea afya njema, lakini vile vile kuwapuuza wanaozusha na kudanganya umma kwa maneno mbalimbali juu ya kutokupanda kwa mishahara ya walimu na kwamba wao wanaamini wataendelea na majadiliano kwa kila changamoto itakayojitokeza na si kuhamasisha maandamano kisha kumaliza kwa kusema, "kupanga ni kuchagua"

Warsha hiyo hufanyika mara moja kila mwaka ilihudhuriwa pia na wadau wa NSSF na NHIF Geita.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa