• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wananchi Jitokezeni Mpate Matibabu

Posted on: November 7th, 2024


Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Ndugu Mohamed Gombati ametoa wito kwa wananchi wote wa Wilaya ya Chato na mkoa mzima kwa ujumla ambao wanasumbuliwa na matatizo ya mifupa, ubongo na mfumo wa fahamu kwenda kuwaona wataalam ili waweze kupatiwa matibabu .

Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita ametoa wito huo tarehe 6/11/2024 alipokuwa akizindua rasmi huduma za kibingwa na ubingwa bozezi za mifupa, ubongo na upasuaji wa mishipa ya fahamu ambazo zinatolewa na Madaktari kutoka Taasisi ya Mifupa na Ubongo (MOI) katika Hospitali ya rufaa ya Kanda Chato.

Ndg. Mohamed Gombati ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwajali wananchi wake na kutoa timu ya wataalam kwa lengo la kuja Mkoani Geita kutoa matibabu ya kibingwa kwa wagonjwa wote wanaosumbuliwa na matatizo ya mifupa, ubongo na mfumo wa fahamu.

“Serikali imetufanyia jambo kubwa sana ambalo limesogeza huduma hizo karibu na wananchi na kuwapunguzia gharama za usafiri, malazi na kero nyinginezo ambazo wangekumbana nazo wanaposafiri kwenda jijini Dar es Salaam kufuata huduma hizo. Hivyo ndugu wananchi wenzangu tumieni kikamilifu fursa hii adhimu ili kupata suluhisho ya matatizo ya kiafya yanayowasumbua”. Aliongeza Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita.


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya MOI, Dkt. Bryson Mcharo ambaye ni Daktari bingwa na mbobezi wa mifupa amesema Serikali kupitia Taasisi ya MOI imekuwa na shauku ya kuhakikisha inawafikishia huduma za kibingwa kwa wananchi wa kanda ya ziwa ili kuwapunguzia umbali wa kusafiri na kusafirisha wagonjwa hadi Dar es Salaam hali iliyopelekea wakati mwingine kuwapoteza ndugu zao wakiwa njiani kufuata huduma hizo . Dkt. Mcharo ameongeza kuwa kwa wiki mbili watakazofanya huduma katika Hospitali ya kanda Chato wamelenga kuwahudumia wagonjwa 300.

Bi. Merina Wilson ni mkazi wa  Wilaya ya Chato na mama anayemuuguza kijana wake ambaye alipata ajali na kuvunjika mguu ametoa shukrani kwa Madaktari bingwa waliotoka MOI ambao wamempatia kijana wake huduma ya kuwekewa vyuma na hali yake inaendelea kuimarika. Pia ameiomba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuweka utaratibu wa kupeleka Madaktari bingwa na wabobezi wa magonjwa mbalimbali ambayo yanawasumbua wananchi.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa