• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wanawake Wahamasishwa Kujihusisha na Sekta ya Madini

Posted on: March 6th, 2025


Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ametoa hamasa kwa wanawake wa Mkoa wa Geita kushiriki kwa wingi katika sekta ya madini kama njia ya kuwakwamua kiuchumi na kuchochea maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Dkt. Gwajima ametoa hamasa hiyo hivi karibuni alipokuwa akizungumza na hadhara ya wanawake waliojitokeza kwa wingi katika Kongamano la kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake ambayo kwa kanda ya ziwa yamefanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Ushirombo Wilayani Bukombe Mkoani Geita.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii amefafanua kuwa wanawake wengi wamekuwa wakijishughulisha baadhi ya kazi za usaidizi katika maeneo mbalimbali ya machimbo na wanachangia sehemu kubwa ya uchumi wa Nchi kupitia sekta ya madini hivyo imefika hatua ya wao kupata fursa sawa na wanaume kwa kupata umiliki wa maeneo ya uchimbaji  ili kujiongezea kipato na kukuza uchumi wa familia na jamii kwa ujumla.

“Serikali ya awamu ya sita imefungua dirisha la uwezeshaji wanawake kiuchumi kupitia mikopo inayotolewa hivyo napenda kutumia fursa hii kuwashauri wanawake wa Mkoa wa Geita kutumia mikopo inayotolewa na Serikali pamoja na Taasisi nyingine za kifedha kukuza Zaidi mitaji yao.” Aliongeza Mhe. Gwajima

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa pongezi za dhati kwa Mhe. Gwajima kwa kuwasaidia wanawake kupata haki na heshima wanayostahili na  kusimamia vyema majukumu ya jumuiya zote zinazofanya kazi kubwa ya kuwaunganisha wanawake wa Mkoa wa Geita. Pia ametoa ombi kwa Taasisi zote za kifedha kuendelea kupunguza riba za mikopo ili wanawake waweze kukopa bila hofu yoyote.

Kongamano la wanawake Kanda ya Ziwa lilibebwa na mada kuu isemayo ushiriki na nafasi ya mwanamke kwenye maendeleo ya Sekta ya Madini ikilenga kuhamasisha wanawake kushiriki Zaidi katika sekta hiyo hususan kwa kanda ya Ziwa ambapo Mkoa wa Geita una vikundi 43 vya wanawake vinavyomiliki leseni za uchimbaji madini na vikundi 20 kupatiwa vitalu vya uchimbaji madini.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa