• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Watumishi wa Afya Geita Tembeeni kifua Mbele” Asema Dkt.Shekalage

Posted on: February 24th, 2022

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita wamelezwa kutakiwa kujivunia mafanikio ya sekta ya Afya kwa kutembea kifua mbele huku wakitambua kuwa Wizara ya Afya inawathamini, inawajali na inawapenda, hivyo wanapaswa kuendelea kufanya kazi kwa mshikamano, umoja na upendo ili kukidhi matarajio ya wateja wao, wakiwemo wagonjwa ili kuhakikisha wanapata huduma iliyo bora katika eneo lao.

Hayo yameelezwa kwao na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalage  Februari 23, 2022 alipokutana na kufanya kikao pamoja nao kwenye eneo la sehemu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa iliyopo mjini Geita akihimiza vilevile kuwa na lugha nzuri ya kuwajali wateja ili taswira nzuri iliyopo isije kuharibiwa.

“kwanza niwapongeze kwa kumpata Dkt. Japhet Simeo Mganga Mkuu Mkoa na Dkt. Mfaume Salum Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa utendaji wao na kuhakikisha hakuna mtumishi anadai madeni ya nyuma. Kama wizara mjue tunawathamini na ndiyo maana tumekuja kuongea nanyi. Lakini pia niwaombe mpendane, mshikamane na mshirikiane ili yote haya yakifanyika kwa pamoja tufikie matarajio ya mteja”. Alisema Dkt.Shekalage.

Aidha Naibu Katibu Mkuu huyo aliwataka watumishi kutambua yakuwa hakuna asiye na thamani kwenye taasisi hiyo, kila mmoja ana thamani na ni wa muhimu na ndiyo maana hufanya kazi kwa kutegemeaana akitumia msemo wa kiiingereza usemao “nobody is useless, everyone is important”  

Awali akiongea na watumishi hao, Mkurugenzi Msaidizi na Msimamizi wa Hospitali za Mikoa kutoka Wizara ya Afya Dkt. Caroline Damian alisema, kwakuwa serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya afya, basi itakuwa ni jambo jema ikiwa kila mmoja atahakikisha huduma zinazotolewa zinaendana na matarajio ya wateja, na hivyo itakuwa ni kuwatendekea haki Wananchi, Wizara na Mhe.Rais kwaniaba ya Serikali bila kusahau matumizi sahihi ya mifumo iliyowekwa kukusanya mapato ili kupunguza utegemezi.

Akisoma taarifa, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Mfaume Salum alisema, pamoja na mafanikio waliyoyapata ikiwemo kulipa stahiki za watumishi na kutoa huduma bora, bado wanahitaji kuboresha miundombinu ya majengo ya zamani wanayoyatumia kwa kipindi hiki yaliyojengwa tangu mwaka 1956 ili kuwa na miundombinu bora zaidi bila kusahau kuiomba wizara kuongeza madaktari bingwa  na gari la kubebea wagonjwa Ambulance.

Awali, Dkt. Shekalage alianza kutembelea maendeleo ya ujenzi wa majengo mbalimbali inapoendelea kujengwa hospitali mpya ya rufaa ya mkoa na kujionea shughuli ya uchimbaji msingi  wa majengo ya wagonjwa mahututi (ICU), jengo la dharura (EMD) na eneo litakapojengwa jengo la mama na mtoto (Maternity Block).


Geita ya Dhahabu, Utajiri na Heshima


Boaz Mazigo

Afisa Habari

Geita RS

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa