• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WATUMISHI WATAKIWA KUTATUA KERO MBALIMBALI ZA WANANCHI GEITA

Posted on: October 30th, 2017

WATUMISHI MKOA WA GEITA WATAKIWA KUTATUA KERO MBALIMBALI ZA WANANCHI

Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel Lughumbi amewataka watumishi na watendaji wa Mkoa wa Geita kufanya kazi kwa juhudi kubwa ili kuleta maendeleo kwa wananchi. Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi kati yake na Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga( Mkuu wa Mkoa Mstaafu)  mheshimiwa Robert  amesema kuwa wananchi wana matarajio makubwa sana na Serikali ya awamu tano hivyo ni lazima kufanya kazi kwa juhudi kubwa. 

"Sikuja kulala nimekuja kufanya kazi lazima tuone mabadiliko ya haraka". Pia amewataka watumishi kutokutumia muda mwingi Ofisini bali waende field ili kuwasaidia wananchi kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula,biashara na kukuza biashara na mitaji ya wafanyabiashara.

Vile vile amewataka viongozi na watumishi kutokubali migogoro na kugawanywa lazima kuishi kwa upendo na umoja ili kufanikisha maendeleo Mkoani Geita kwa kuwa maendeleo ya Geita yataletwa na sisi wenyewe.

Mkuu wa Mkoa amemshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuwaletea wananchi wa Geita maendeleo kwa kipindi chote ambacho amekuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita. Kwa upande wake Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa Mstaafu amemweleza Mkuu mpya wa Mkoa kuwa wananchi wa Geita ni wachapakazi wanalima mashamba makubwa ili kujiletea maendeleo na wanashiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Mheshimiwa Robert Gabriel Lughumbi anakuwa Mkuu wa Mkoa wa nne katika Mkoa wa Geita tangu Mkoa huu kuanzishwa mwaka 2012 akifuata watangulizi wake Magalula Said, Fatma Mwassa na Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa