• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Waumini wa Dini Zote Waaaswa Kudumisha Upendo

Posted on: March 28th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela amewaasa waumini wa dini zote katika Mkoa wa Geita kuendeleza utamaduni wa kuthaminiana, kuheshimiana, kushirikiana na kupendana katika hali zote.

Mhe. Shigela ametoa ujumbe huo hivi karibuni alipokuwa akizungumza na waumini wa dini ya kiislam pamoja na dini nyingine wakati wa Iftari maalum aliyoiandaa kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wake katika ukumbi wa Shule ya Sekondari St. Aloysius Geita mjini.

Mkuu wa Mkoa wa Geita aliongeza kuwa mwaka 2025 umekuwa mwaka wa neema ya ajabu kwa sababu waumini wa dini zote kwa maana ya waislam na wakristo wamefunga kwa wakati mmoja, hivyo watu wote hawana budi kuzidi kuomba Amani, umoja na mshikamano vidumu katika Nchi yetu hususan katika mwaka huu tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Mhe. Shigela ametumia fursa hiyo pia kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwjaengea wananchi wake msingi wa Amani, upendo, utulivu na mshikamano pamaoja na kuendelea kuufungua mkoa wa Geita kimaendeleo kupitia ujenzi wa daraja la Kigongo- Busisi, ujenzi wa barabara za lami kuunganisha mikoa na kutoa fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Geita Nicholaus Kasendamila amepongeza jambo la imani lililofanywa na Mkuu wa Mkoa na kushauri jambo hilo liwe endelevu na la kuigwa kwa viongozi wote, pamoja na kuwakumbusha viongozi wa dini kuzidi kuwakumbuka katika dua na maombi yao viongozi wote wa Serikali katika kutimiza majukumu yao ya kila siku.

Wakitoa neno la shukrani, Viongozi wa Baraza la Waislam Mkoa wa Geita wametoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kwa namna anavyoshirikiana  nao katika majukumu mbalimbali ya kiserikali pamoja na migogoro inayohitaji kufanyiwa usuluhishi bila ubaguzi wa aina yotote.

“ Mtu anayefanya mema ni lazima apongezwe, Mkoa wa Geita tuna bahati ya kumpata Mkuu wa Mkoa ambaye amewaunganisha viongozi wote wa Dini ambao wanaketi na kujadili masuala mbalimbali muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu.” Waliongeza viongozi wa BAKWATA.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa