• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

Posted on: April 15th, 2025


Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ametoa agizo kwa Mgodi wa Dhahabu Geita( GGML) kuketi na Wakurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita na Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa lengo la kuandaa na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Miradi ya CSR kuanzia mwaka 2018 hadi 2021.

Mhe. Mavunde ametoa agizo hilo tarehe 14 Aprili 2025 wakati wa kikao cha kujadili utekelezaji wa Miradi ya Mpango wa Uwajibikaji wa Kampuni ya GGM kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Wizara ya Madini jijini Dodoma.

Waziri wa Madini ameeleza kuwa ameitisha kikao hicho kwa lengo la kutafuta njia bora ya kutekeleza miradi ya CSR, kutatua changamoto zilizopo na kuhakikisha wananchi wa Geita wananufaika na rasilimali madini yanayochimbwa katika maeneo yao.

“Wananchi wa Geita wanatamani kuona matokeo ya moja kwa moja ya uwepo wa mgodi huo kwa kupitia miradi ya maendeleo, hivyo kuna umuhimu wa kukamilisha utekelezaji wa miradi ya nyuma kuanzia mwaka 2018-2021 ili kuwezesha uanzishwaji wa miradi mipya yenye tija kwa jamii.” Aliongeza Mhe. Mavunde

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela amehimiza ushirikiano wa karibu baina ya GGML na Serikali kwa kuwasisitiza GGML kuhakikisha miradi iliyosainiwa inatekelezwa kwa wakati na kwa mujibu wa makubaliano ili wananchi wa Geita waweze kunufaika.

Wakichangia maoni Wabunge wa majimbo ya Geita mjini, Geita Vijijini na Busanda wameitaka kampuni ya GGML kuhakikisha inakamilisha miradi ya CSR kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu utakaoendana na gharama zilizotumika ili wananchi wa Geita wayaone matunda ya uwepo wa Mgodi huo.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Anglo Gold Ashanti Ndg. Simon Shayo amesema kwamba Kampuni ya GGML iko tayari kushirikiana na uongozi wa Mkoa wa Geita ili kuhakikisha wananchi wa Geita wananufaika na miradi ya CSR ambayo kwa sasa kiasi cha Shilingi Bilioni 21 imetekwa kwa ajili ya utekelezaji na ukamilishaji wa miradi ya kuanzia mwaka 2018 hadi mwaka 2024 ambayo ilikuwa imekwama kwa sababu ya changamoto mbalimbali.

Kikao hicho kimehusisha viongozi kutoka Wizara ya Madini, Tume ya Madini, Uongozi wa Mkoa wa Geita, Wabunge wa Wilaya ya Geita pamoja na wawakilishi wa GGML kwa nia ya kupata muafaka kuhusu changamoto za utekelezaji wa miradi ya CSR na kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha wananchi wa Geita wananufaika na uwepo wa Mgodi huo.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa