• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

VIWANDA NA BIASHARA

Mkoa wa Geita unazo fursa mbalimbali za Kiuchumi ambazo kimsingi ndizo zimekuwa zikichochea ukuaji wa sekta ya viwanda katika mkoa. Fursa hizo za Kiuchumi zimejikita katika shughuli kuu za uzalishaji mali za kilimo, ufugaji, uchimbaji madini ya dhahabu, uvuvi na baishara ndogondogo. Mkoa unatekeleza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuwa na Uchumi wa Viwanda hususani viwanda vidogo katika Mkoa ni sekta muhimu katika kutengeneza ajira, kukuza kipato na kuondoa umasikini.

Mkoa una jumla ya viwanda 791, ambapo viwanda viidogo ni 521, vya kati ni 269 na viwanda vikubwa vitatu (03). Sekta ya kilimo ndio inayoongoza kwa uwekezaji wa viwanda vya usindikaji wa mazao hususan mazao ya nafaka hasa usindikaji wa mahindi ukifuatiwa na zao la mpunga. Aidha, uwekezaji mkubwa ni shughuli ya kukoboa mpunga na kusaga mahindi ambapo kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 1 inakadiriwa kuwekezwa.

Sekta mpya katka uwekezaji wa viwanda ni pamoja na usindikaji wa mafuta ya alizeti na unenepeshaji wa mifugo hususan ng’ombe wa nyama unaofanyika wilayani chato. Pia zao la Pamba limeonesha kufufua matumaini ya uwekezaji katika viwanda vya kuchambua pamba ambapo mkoa una jumla ya viwanda (02) vya kuchambua Pamba vinavyofanya kazi, viwanda hivyo ni KCCL kilichopo wilaya ya Geita na BCU katika Wilaya ya Chato.

Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) 

Mkoa unayo Ofisi ya kuhudumia viwanda vidogo ambayo imeanzishwa mwezi Desemba 2015. Katika kutekeleza majukumu yake Ofisi hiyo imekuwa ikitoa huduma mbalimbali kwa wajasiriamali kama ifuatavyo:-

Kuendeleza/ Kuleta teknolojia mbalimbali katika Mkoa huu kama vile mitambo ya kusindikaalizeti na utengenezaji sabuni.

  • Kuwaunganisha wajasiriamali na Masoko
  • Kutoa mikopo kwa wajasiriamaliwadogo  na wakati
  • Kutoa mafunzo ya uanzishwaji wa viwanda, uboreshaji wa takwimu za viwanda na uzingatiaji wa viwango na ubora wa bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali kwa kushirikia na Mkoa.
  • Kuzihamasisha Mamlaka za serikali za Mitaa kutenga maeneo kwa ajili ya viwanda vidogo.

Mkoa unayo mikakati ifuatayo katika kuendeleza sekta ya viwanda:-

Kuanzisha kiwanda cha kuchakata muhogo na kufungasha ambapo maghala (02) ya kuhifadhi muhogo na soko (01) yamejengwa na Kukamilika kupitia Programu ya uboreshaji wa miundombinu ya masoko uongezaji thamani na huduma za kifedha vijijini (MIVARF). Vikundi vya wazalishaji vimekutanishwa na benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania (TADB) kwa ajili ya kupewa mkopo na andiko la Mradi linaandaliwa.

Kufufua kiwanda cha kuchambua Pamba cha Kasamwa Geita ambapo hatua iliyofikiwa sasa ni kuwa NCU (1984)LTD inashirikiana na Mifuko ya hifadhi ya jamii kwa ajili ya kufunga vyerehani vipya 20 aina ya Bajaj ili Pamba iliyozalishwa msimu huu 2017/2018 iweze kuchambuliwa.

Kuhamasisha na kuandikisha Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Geita ambacho kitahusisha Wilaya za Geita,  Nyang’hwale, Bukombe na Mbogwe kwa ajili ya kusogeza huduma za uzalishaji wa mazao ya biashara kwa wakulima na kuboresha masoko ya mazao yao.

Kuanzishwa kiwanda cha kusindika nyama katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe ambapo andiko limeandazliwa na kuwasilishwa katika Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji kwa ajili ya kupata mwekezaji.

Ujenzi wa Kiwanda cha sukari Nyamwilolelwa/Chigunga eneo la ekari 100 limetengwa na serikali ya kijiji cha Chigunga. Eneo la hekta 6,000 sawa na ekari 14,826 zinazomilikiwa na wakulima zitatumika kuzalisha miwa. Halmashauri ya wilaya ya Geita imetenga shilingi bilioni 1.402 kwa ajili ya kiwanda hicho mwaka 2018. Kiwanda kitaendeshwa kwa ubia baina ya Halmashauri ya Wilaya na Bodi ya sukari Tanzania.

Kuanzisha kiwanda cha kufungasha mazao ya nyuki (Asali na Nta)_ katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe. Uhamasishaji wa vikundi vya wafugaji wa nyuki kujiunga pamoja ili vitambulike kisheria na viweze kukidhi vigezo vya kukopsheka umefanyika.

Kutangaza fursa za kilimo cha mpunga kwenye mabonde yaliyopo wilaya ya Chato na Geita kwa wawekezaji ambao wako tayari kuweka miundombinu ya umwagiliaji kwa kutumia maji ya ziwa Victoria.

Kuanzishwa kwa Supermarket katika Mji wa Geita ambayo itauza bidhaa za viwanda vidogo zinazozalishwa na wajasiriamali wa Mkoa wa Geita. Eneo limeshapatikana katika soko jipya linalojengwa katika mjia wa Geita.

Uanzishwaji wa kiwanda cha Nyama – Chato ambacho kinaanzishwa na Kampuni  ya Kahama oil Mills (KOM) ambapo eneo la ekari 1000 limepatikana katika kijiji cha Itale kiwanda kitapokamilika kitakuwa na uwezo wa kuchinja ng’ombe 700 kwa siku.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2022 YATOKA January 29, 2023
  • KARIBU UPATE FOMU YA USHIRIKI KWENYE MAOENSHO YA TANO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2022 September 11, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) PARTICIPATION FORM September 12, 2022
  • THE 5TH TANZANIA MINERALS TRADE FAIR (TMTF) SPONSORSHIP PACKAGES September 11, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Shigela Asisitiza Mambo Matatu, Kiapo cha Ma DC Geita

    January 30, 2023
  • RC Shigela Asisitiza Mambo Matatu, Kiapo cha Ma DC Geita

    January 30, 2023
  • “Mgogoro wa Shambani Humalizwa Shambani”. Asema RC Shigela.

    December 29, 2022
  • RC Shigela Akabidhi Zawadi za Rais Samia

    October 16, 2022
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa