• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Visima 150 Kuwanufaisha Wakulima Mkoani Geita

Posted on: October 17th, 2025


Mradi wa visima virefu 150 vya kilimo cha umwagiliaji vitakavyojengwa katika Halmashauri zote za Mkoa wa Geita utawanufaisha wakulima kwa kulima kilimo cha uhakika kupitia umwagiliaji kwa mwaka mzima.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo uliofanyika tarehe 16 Oktoba 2025 katika Kijiji cha Mwilima Kata ya Kanyala, Manispaa ya Geita, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita imefanya jambo la kukumbukwa na wakulima wa Mkoa wa Geita kwa sababu baada ya ujenzi wa visima hivyo watakuwa na uhakika wa kufanya shughuli za kilimo katika kipindi chote cha mwaka.

Mhe. Shigela amewasisitiza wakulima wa eneo la Kanyala na wilaya nyingine za Mkoa wa Geita kuutunza na kuuthamini mradi wa visima hivyo ambavyo vitawawezesha kuongeza uzalishaji wa mazao kupata kipato endelevu.

“Natoa wito kwa maafisa ugani wote kufanya utafiti wa udongo kwa ajili ya kuwaletea wananchi pembejeo zinazoendana na ardhi ya maeneo ya kilimo. Pia Serikali ya awamu ya sita imejipanga kuleta masoko na kujenga maghala sambamba na kuleta stakabadhi za mauzo hivyo mjipange kunufaika na mazuri yanayofanywa na Serikali yenu.” Aliongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Kwa upande wake Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Geita Boniphace Mitika amesema kuwa mradi wa visima vya kilimo cha umwagiliaji vinatekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ambapo kwa awamu ya kwanza Mkoa wa Geita utatekeleza visima 36 katika vijiji 32 vyenye jumla ya ekari 1440 lenye zaidi ya wakulima 747.

Mhandisi Mitika ameongeza kuwa upatikanaji wa maji ya uhakika utaongeza uzalishaji wa mazao kwa kiwango kikubwa na kumpatia faida mkulima mdogo Pamoja na upatikanaji wa chakula cha kutosha kuanzia ngazi ya kaya hadi Taifa na kuwainua wakulima wadogo n awa kati kiuchumi.

Mradi wa uchimbaji visima virefu  vya kilimo cha umwagiliaji umeibuliwa kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wakulima wadogo kupitia kilimo cha umwagiliaji. Mradi huu unasimamiwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wenye thamani ya Shilingi Bilioni 37.34



Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Visima 150 Kuwanufaisha Wakulima Mkoani Geita

    October 17, 2025
  • Wakandarasi wa Maji Watakiwa Kukamilisha kazi kwa Wakati

    October 15, 2025
  • Maendeleo yote Yanaletwa na Walimu- Waziri Mkuu

    October 04, 2025
  • Sekta ya Madini Yapaisha Pato la Taifa- Dkt. Biteko

    September 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa