• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Sekta ya Madini Yapaisha Pato la Taifa- Dkt. Biteko

Posted on: September 28th, 2025


Mchango wa Sekta ya Madini katika pato la Taifa umeongezeka kutoka asilimia 6.8 mwaka 2020 hadi kufikia asilimia 10 mwaka 2024 huku mchango wa wachimbaji wadogo na mapato yote ya sekta ya madini ukiongezeka kutoka asilimia 20 mwaka 2020 hadi asilimia 40 mwaka 2024.

Takwimu hizo zimetolewa na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko alipokuwa akizungumza na hadhara ya wananchi wa Mkoa wa Geita wakati wa ufungaji rasmi wa Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini 2025.

Dkt. Biteko ameeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na jitihada za Serikali kuongeza ushirikishwaji wa watanzania katika sekta ya Madini ikiwa ni Pamoja na shughuli zote za mnyororo mzima wa thamani ya Madini Nchini, ambapo kwa Mkoa wa Geita pekee wachimbaji wadogo wamezalisha kilo 22,014.61 zenye thamani ya shilingi trilioni 3.43 na Serikali kukusanya mapato ya shilingi Bilioni 2.5 katika kipindi cha mwaka 2021/22 hadi 2024/25.

“Natumia fursa hii kuwapongeza wachimbaji wadogo,kati, wakubwa na Wizara ya Madini kwa mafanikio hayo yaliyowezesha kuinua pato la Taifa. Natoa wito kwenu kuendelea kubuni teknolojia za juu zaidi na kuongeza uwezeshwaji wa watanzania kuongeza thamani ya Madini wanayozalisha, mazingira hayo yataongeza upatikanaji wa fedha za kigeni Pamoja na kuwapatia watanzania kuongeza thamani ya Madini wanayozalisha.” Aliongeza Dkt. Biteko.

Naibu Waziri Mkuu amewahakikishia wadau wote wa sekta ya Madini kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya Madini ikiwemo kufikisha huduma ya umeme katika maeneo yote yanayohitaji huduma hiyo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Ndg. Msafiri Mbibo amesema kuwa Wizara ya Madini itaenbdelea kusimamia sheria na taratibu zote ili kuifanya sekta hiyo kutoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa Taifa. Pia ameeleza namna Maonesho ya Teknolojia ya Madini yalivyokuwa chachu hususan kwa wachimbaji wadogo kwa kuwaongezea elimu kuhusu uchimbaji hatarishi na matumizi ya zebaki.


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kutolewa kwa leseni 9,000 kwa wachimbaji wadogo wakiwemo wa pori la Kigosi ikiwa ni hatua ya Serikali katika kuhakikisha wachimbaji wadogo wanapata maeneo yatakayowapa fursa ya kujikwamua kiuchumi.

Maonesho ya Teknolojia ya Madini 2025 yamebebwa na Kauli Mbiu isemayo ‘Ukuaji wa Sekta ya Madini ni Matokeo ya Matumizi ya Teknolojia Sahihi na Uongozi Bora, Shiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025.’ Jumla ya washiriki 930 wakiwemo washiriki kutoka nje ya Nchi wameshiriki ikilinganishwa na washiriki 600 waliokuwepo mwaka 2024.



Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Sekta ya Madini Yapaisha Pato la Taifa- Dkt. Biteko

    September 28, 2025
  • Wadau na Wananchi Geita Waaswa Kuendeleza Sekta ya Madini

    September 25, 2025
  • Fursa Zitolewazo na Serikali Kunufaisha Wajasiriamali Wadogo

    September 23, 2025
  • Wafugaji Waaswa Kujali Afya ya Punda

    September 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa