• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wakandarasi wa Maji Watakiwa Kukamilisha kazi kwa Wakati

Posted on: October 15th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa wito kwa wakandarasi wote waliofanikiwa kusaini mikataba minne ya ujenzi wa miradi ya maji yenye thamani ya shilingi Bilioni 3.6 za Kitanzania ambayo itatekelezwa kwenye vijiji 12 katika Wilaya za Chato, Geita na Mbogwe.

Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo hivi karibuni alipokuwa anashuhudia zoezi la utiaji Saini wa mikataba hiyo baina ya Wakandarasi watakaofanya kazi hiyo na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA). Hafla ambayo ilifanyika katika ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita ametumia nafasi hiyo kuwapongeza wataalam wa RUWASA kwa kuhakikisha wanaifanyia kazi maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumtua mama ndoo kichwani, na kuongeza kuwa baada ya kukamilika kwa miradi hiyo Mkoa wa Geita utafikisha asilimia 86% ya utoaji huduma ya maji.

“Miradi hii itakapokamilika kwa wakati uliokusudiwa utawawezesha wananchi kunufaika nayo na kuondokana na kero ya kufuata maji katika vijiji Jirani mbali na makazi yao na kuufanya Mkoa wa Geita kuondokana na tatizo la ukosefu wa maji safi na salama.” Aliongeza Mhe. Shigela.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini( RUWASA) Mkoa wa Geita, Mhandisi Jabiri Kayilla ameeleza kuwa miradi hiyo yam aji inatarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji vijijini kwa asilimia nne, ambapo kwa sasa hali ya upatikanaji wa maji katika maeneo ya vijijini ni zaidi ya asilimia 70% na baada ya utekelezaji wa miradi hiyo kukamilika Mwezi Aprili 2026 hali ya upatikanaji maji itaongezeka na kufikia asilimia 86%.

Miradi minne ya maji itakayotekelezwa katika vijiji vya Lwezera, Ikina, Bugogo, Ihega, Nyarugusu, Rumasa, Mabila, Ngemo, Bwendamwizo, Ilolangulu, Buningozi na Mpakali itatoa huduma kwa wananchi wapatao 27,000 wa maeneo hayo.


Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wakandarasi wa Maji Watakiwa Kukamilisha kazi kwa Wakati

    October 15, 2025
  • Maendeleo yote Yanaletwa na Walimu- Waziri Mkuu

    October 04, 2025
  • Sekta ya Madini Yapaisha Pato la Taifa- Dkt. Biteko

    September 28, 2025
  • Wadau na Wananchi Geita Waaswa Kuendeleza Sekta ya Madini

    September 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa