• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Bandisa Anena na Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Geita, Awang'ata Sikio Siri ya Mafanikio.

Posted on: October 9th, 2018

Katika kuhakikisha watumishi wa Umma Mkoani Geita wanafanya kazi na kuleta matokeo, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Denis Bandisa amekutana na kufanya kikao na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 08.10.2018 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Hiki ni kikao cha kwanza cha Kimkakati ambacho Bw. Bandisa anakitumia kuwahamasisha watumishi kufanya kazi kwa bidii ili kutekeleza Dira na Dhima ya Mkoa ambayo hupelekea matokeo kwenye utekelezaji wa shughuli za serikali na kuwahudumia wananchi.

Amesema, “moja ya mambo yanayopelekea mafanikio ni Ushirikiano, kwakuwa watu wanaoshirikiana hujenga, ni rahisi kufanikiwa kwa kuwa kila mmoja atajiona ni mhusika, hivyo nahimiza ushirikishwaji baina ya idara na idara ili kila mmoja apte nafasi ya kutoa matokeo”.

Ameongeza kusema kuwa, watumishi wa Umma sharti wawe na Weledi na  Ujuzi hata kwa kuongeza elimu. Amewashauri kupenda kujiendeleza kielimu kwakuwa elimu haina mwisho, vilevile hata wanaopenda kupandishwa vyeo ni muhimu kujiimarisha kitaaluma.

Bw. Bandisa pia amewakumbusha watumishi juu ya kuwa na nidhamu kazini, tabia nzuri, majibu mazuri kwa wateja na kusema kuwa unyenyekevu ni dawa pale unapomhudumia mteja ama mwananchi.

Mwisho, watumishi wamehimizwa juu ya uwazi na kutokuwa wabinafsi katika kutumia rasilimali zilizopo katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku bila kusahau uwajibikaji akisisitiza kuwa unaanzia hata nyumbani kwamba, kama hata mtoto asipofundishwa vizuri tangu angali mdogo ni vigumu kuwajibika hata akiwa mkubwa kwa kuwa siku zote yatupasa kutambua kuwa, “HAKUNA HAKI BILA WAJIBU”, kisha akakalibisha michango na changamoto kutoka kwa watumishi hao.


Watumishi wakampongeza Bw. Bandisa kwa kufanya kikao pamoja nao wakisema kuwa huu ni mwanzo mzuri kwakuwa endapo watakuwa na changamoto wataziwasilisha kwa ajili ya utatuzi ikiwa lengo lao ni kuufikisha mkoa kwenye malengo uliojiwekea katika kufikisha huduma kwa jamii pia wakaahidi kufanyia kazi yote waliyoelekezwa.

Hakika Geita ni ya Amani, Umoja na Kazi.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa