• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Bilioni 38 Kutumika Mradi wa Majisafi Miji 28-Chato

Posted on: August 25th, 2023

Na Boazi Mazigo-Geita RS

Katika sura ya kwanza, ibara ya 9 (D)(i) ya ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 imeeleza wazi juu ya Kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za Afya, Elimu, Maji, Umeme na Makazi vijijini na mijini ikisema, “Kuongeza kasi ya usambazaji majisafi na salama ili kutosheleza mahitaji kwa zaidi ya asilimia 85 vijijini na zaidi ya asilimia 95 kwa mijini, kwa upande wa Tanzania Bara, ifikapo mwaka 2025, na zaidi ya asilimia 95 kwa upande wa Zanzibar”.  Sura hiyo imeifanya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa Geita kupita, kutembelea na kujionea hali ya utekelezaji wa mradi wa majisafi wa miji 28 unaotekelezwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wa Maendeleo kupitia program ya Maendeleo ya sekta ya maji nchini (WSDP 2006-2025) kwa gharama ya Dola za kimarekani Milioni 16.493 sawa na shs.bilioni 38, mradi ulioanza Aprili 11, 2023 na kutarajiwa kumalizika Desemba 10, 2025.

Kamati hiyo iliyotembelea eneo la mradi Agosti 24, 2023 imesema, ipo haja ya kupanua zaidi huduma hiyo ya maji tofauti na ilivyokuwa imekisiwa kutokana na kuonekana fedha hiyo inaweza kuhudumia eneo kubwa zaidi ya lile lililoanishwa.

Akiongea akiwa kwenye eneo la mradi, mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Mkoa Geita Nicholaus Kasendamila alisema, " nikupongeze mkuu wa wilaya mhe.Deusdedith Katwale pamoja na wizara ya maji kwa kuona umuhimu wa kusogeza huduma ya maji mbele zaidi ya mradi ulipokuwa umekisiwa na kuwa na ndoto ya kufikisha maji hayo kata ya Bwanga. Pia hakikisheni hakuna mwananchi yeyote anadai fidia ili kazi ifanyike vizuri. mwisho nimpongeze kwa dhati Rais wetu Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wananchi anaowaongoza wakiwemo wa mkoa huu na wilaya ya Chato pia, tuendelee kumuunga mkono"

Akisoma taarifa ya mradi, afisa mazingira kutoka CHAWASSA bi. Jesca Salima alisema ujenzi wa mradi huo utahusisha ujenzi wa chanzo (Intake) chenye ukubwa wa lita 11,000,000 kwenye ziwa Victoria, ujenzi wa chujio (WTP) lenye ukubwa wa kuzalisha lita 10,000,000 kwa siku, ujenzi wa kuhifadhia maji eneo la Katende Hill lenye ujazo wa lita 3,000,000, ulazaji wa bomba kuu lenye kipenyo cha 300mm hadi 400mm urefu wa Km.36 kutoka chujio hadi kwenye tanki la Katende na kuyapeleka mjini kwenye matanki yaliyopo (Itale, Mlimani, Hospitali na Kiwandani pamoja na ulazaji wa mabomba ya usambazaji wa maji yenye vipenyo vya milimita 75 hadi 400 urefu wa km.30

Bi.Salima aliongeza kuwa, kata zitakazonufaika na mradi huo ni Ilemela, Katende, Ilyamchele, Bukome, Nyamigogo, Muungano, Chato, Bwina na Nyamirembe, na kwamba mradi utakapokamilika utaongeza upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama kutoka asilimia 85 hadi 100 kwa mji wa Chato.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa