• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wadau na Wananchi Geita Waaswa Kuendeleza Sekta ya Madini

Posted on: September 25th, 2025


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa amewaasa wadau pamoja na wananchi wote wa Mkoa wa Geita kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha sekta ya Madini kwa maendeleo ya Taifa.

Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito huo alipokuwa akizungumza na hadhara ya wananchi waliojitokeza kwa wingi kuhudhuria hafla ya uzinduzi wa Maonesho ya nane ya Teknolojia ya Madini tarehe 22 Septemba 2025 katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan Bombambili Geita Mjini.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameeleza kuwa sekta ya Madini ni injini muhimu ya maendeleo ya Taifa na inaweza kuleta manufaa makubwa kwa kizazi cha sasa na kijacho iwapo itaendelezwa kwa weledi, uwazi na uadilifu.

“Leo hii Mkoa wa Geita unapata heshima kuwa mkoa unaoongoza kwa uzalishaji wa dhahabu Nchini,hii imewavutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza na matokeo yake mji unazidi kukua kwa kasi na maisha ya wananchi yameendelea kuboreka na Serikali inaahidi kuendelea kutoa ushirikiano katika kuendeleza Sekta ya Madini”. Aliongeza Mhe. Waziri Mkuu.

Akizungumza katika ufunguzi huo Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ameeleza kuwa katika kutekeleza agizo la viongozi wakuu waliofika katika Maonesho ya miaka ya nyuma tangu yalipoanzishwa ambapo waliagiza kujengwa kwa miundombinu ya kudumu, mwaka huu majengo tisa ya kudumu yamejengwa kupitia misingi ya watu wanaopendana, kuheshimiana na kuthaminiana hatimaye kupelekea kufanikisha ujenzi wa awali wa miundombinu ya kudumu.

Mhe. Shigela ameongeza kuwa Mkoa wa Geita umefanikiwa kuzalisha kilo 22,000 za madini ya dhahabu zenye thamani ya shilingi trilioni 3.4 kutoka kwa wachimbaji wadogo ndani ya kipindi cha mwaka 2021 hadi 2025 na Serikali kupata mrabaha wa Shilingi Bilioni 235.5 Kadhalika ndani ya kipindi cha uongozi wa Serikali ya awamu ya sita leseni za wachimbaji wadogo zimefikia 9000 mwaka 2025 kutoka leseni 900 kwa mwaka 2021.




Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Sekta ya Madini Yapaisha Pato la Taifa- Dkt. Biteko

    September 28, 2025
  • Wadau na Wananchi Geita Waaswa Kuendeleza Sekta ya Madini

    September 25, 2025
  • Fursa Zitolewazo na Serikali Kunufaisha Wajasiriamali Wadogo

    September 23, 2025
  • Wafugaji Waaswa Kujali Afya ya Punda

    September 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa