• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

BODA BODA WASIOVAA KOFIA NGUMU KUKAMATWA- GEITA

Posted on: December 8th, 2017

BODA BODA WASIOVAA KOFIA NGUMU  GEITA KUKAMATWA 

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi amemuagiza Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani  Mkoa wa Geita Alfred Hussein kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria waendesha pikipiki wote wasiovaa kofia ngumu maarufu kama ''helmet'' wanapotimiza majukumu yao ya usafirishaji wa abiria.

Akizungumza katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambayo kimkoa yanafanyika Mji mdogo wa Katoro Wilaya ya Geita Mheshimiwa Robert Gabriel amesema muendesha piki piki yeyeto asiyevaa kofia ngumu Mkoani humu  akamatwe na kuwekwa ndani ili liwe fundisho kwa watu wote wasiopenda kutii sheria na matokeo yake wanasababisha vifo kwa jamii. "Naamini kuanzia wakati huu RTO na Kamati za Usalama barabarani Mkoa na Wilaya mtu asiyevaa kofia ngumu atakamatwa na kuwekwa ndani tutatumia sheria zote hakuna kupatana hakuna kuelewana". Ameongeza kuwa watumiaji wa vyombo vya moto wanatakiwa kuelimishwa na kufundishwa taratibu zinazowaongoza katika utumiaji wa vyombo hivyo na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi pamoja na vyombo vyao wapate elimu ili kujua mbinu za kuwafanya kuwa salama.

Mhandisi Robert Gabriel amewataka abiria kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama pamoja na kutowaruhusu madereva kuendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi kwa kuwa jukumu la Usalama ni la kila mwananchi.

Aidha, amekipongeza kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa kwa kazi nzuri ya kuzingatia usalama wa wananchi katika barabara,  amewataka waendelee kusimamia suala hili na kuchukua hatua pale inapobidi.

Awali Mkuu wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa ndugu Alfred Hussein alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa kuwa ajali za barabarani zimepungua kutoka ajali 87 mwaka 2016 hadi kufikia ajali 68 kwa mwaka huu. Vile vile ameeleza kuwa idadi ya vifo pia imepungua kutoka vifo 98 mwaka 2016 hadi vifo 79 kwa mwaka huu wa 2017.

Alfred ameongeza kuwa kwa ajali nyingi zinasababishwa madereva kuendesha vyombo vya moto wakiwa wametumia vilevi mbalimbali, mwendo kasi, kukosa umakini barabarani, uchakavu wa vyombo vya usafiri na miundombinu.  Maadhimisho haya yanafanyika kwa wiki nzima ambapo wananchi, madereva na wamiliki wa vyombo vya moto wanapata elimu kwa lengo la kuhakikisha kila mtu anajikinga na ajali za barabarani.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara Wadogo Wahamasishwa Kujisajili

    May 15, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa