• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

BUCREEF Yatoa CSR ya Milioni 420 Wilayani Geita

Posted on: April 28th, 2023

Na Boazi Mazigo- Geita

Neema inaendelea kumwagika mkoani Geita kwenye awamu ya sita ya uongozi wa Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo viongozi mbalimbali wameshuhudia utiaji saini makubaliano ya utekelezaji mpango wa wajibu wa kampuni kwa jamii CSR ya shilingi milioni 420 kati ya Mgodi wa Bucreef unaojihusisha na uchimbaji madini ya dhahabu na halmashauri za wilaya na mji Geita.

Mkuu wa mkoa Geita Mhe.Martine Shigela ameshuhudia zoezi hilo Aprili 27, 2023 katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa na kuupongeza mgodi huo huku akitoa wito kwa wawekezaji wengine kuja kuwekeza mkoani hapa kisha kuagiza utekelezaji wa miradi ya CSR kuzingatia muda.

“hongereni sana Bucreef, hii ni fursa ya wanaGeita kuchangamka, tusizubae, tutumie fursa ya utekelezaji miradi ya CSR tuwe kwenye mnyororo wa thamani. Haya ni matokeo ya kupanua uwekezaji na juhudi hizi zinahimizwa na Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri ambayo hata sisi Geita tumeendelea kufanya hivyo. Matarajio yangu ni kuwa, miradi iliyosainiwa leo itakamilika kabla ya mwezi novemba, 2023 na hata mchakato wa utekelezaji wa miradi ya CSR kutoka makampuni mengine ianze mapema mwishoni na mwaka huu”, alisema Mhe.Shigela

Aliongeza kuwa, mkoa utaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji na hivyo anatoa wito kuwaalika wawekezaji mkoani Geita kwa uwekezaji endelevu.

Meneja mkuu wa mgodi wa Bucreef Bw.Gaston Mujwahuzi alisema “tunaanza na CSR ya Milioni 420 kwa mwaka 2022/2023 na CSR yetu itahusika kwenye sekta ya elimu, afya na mazingira. Tunaamini mwakani kiwango kinaweza kuongezeka nasi tukachangia kiasi kikubwa kwa sababu kwa sasa tunazalisha Tani 45 kwa Saa kwa Sasa na mwaka 2024 tunatarajia kuongeza uzalishaji kufikia tani 90 hadi 100 kwa saa, hivyo tunaomba ushirikiano”

Kwa upande wake katibu tawala mkoa Geita Prof.Godius Kahyarara ameupongeza mgodi huo kwa kutekeleza mojawapo ya takwa la kisheria kuwajibika kwa jamii hivyo kusisitiza kuwa matokeo ni muhimu kwakuwa jamii inatarajia kuona kilichofanyika kutokana na makubaliano yaliyofikiwa kwenye  utekelezaji wa miradi ya CSR.

Mkuu wa wilaya Geita Mhe.Cornel Magembe alitumia fursa hiyo kumpongeza Mhe.Shigela kwa kuwa sehemu ya kuwahimiza wawekezaji kutimiza jukumu hilo la kisheria akisema ni matarajio yake kuwa Bucreef pamoja na halmashauri za wilaya anayoiongoza watawajibika na kwamba wahakikishe miradi yote inatekelezwa na inakamilika kwa wakati akisema, “niko tayari kusimamia utekelezaji wa CSR hii”

Mgodi wa Bucreef unaundwa na Shirika la Madini la Taifa STAMICO kwa 45% na kampuni ya TRX Gold Canada kwa 55% na hufanya shughuli zake za uchimbaji wilayani Geita.


CSR Kututoa Kimasomaso Wana Geita



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa